Posts

Image
 xxxxxxxxxxxxxxxxxx Mama Samia Legal Aid Campaign Yaweka Kambi Arusha. Timu ya watoa Huduma za Msaada wa Kisheria kupitia Kampeni ya "Mama Samia Legal Aid" imeweka kambi rasmi Machi 27, 2025 Jijini Arusha, ikiwa ni muendelezo wa kuihudumia Jamii inayokabiliwa na uhitaji wa Msaada wa Kisheria. Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda amewashauri watumishi wa Samia Legal Aid kuwa wasikivu na kutanguliza utu wanaposhughulikia kero za Wananchi, kwani wanamwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye shauku yake kubwa ni Wananchi kutatuliwa changamoto zao. "Mnatakiwa kuwa wasikivu na kutanguliza utu mnaposhughulikia kero za wananchi, kwani mnamwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye shauku yake kubwa ni wananchi kutatuliwa changamoto zao." Mhe. Makonda amesema hayo wakati akiongea na wataalam wa Sheria wakiwemo mawakili, maofisa maendeleo ya jamii pamoja na wakuu wa idara na vitengo mbalimbali waliokutana kwaaajili ya kupanga mikakati ya utatuzi wa cha...

WATENDAJI WA KATA KUWENI WAZALENDO KWA MASLAHI YA TAIFA

Image
  xxxxxxxx Watendaji wa kata wa Wilaya ya Mkinga wametakiwa kuwa wazalendo kwa kuacha tabia ya kuwasaidia raia wa kigeni kupata vitambulisho bila kufuata taratibu za nchi kwa kuwa kufanya hivyo ni hatari kwa mustakabali wa Taifa. Rai hiyo imetolewa na Afisa Tawala Mwandamizi Erick Farahani wakati alipomwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Mhe. Gilrbet Karima katika kufungua Mafunzo ya Uraia na Utawala Bora kwa Kamati ya Usalama Wilaya, Wakuu wa Idara na Watendaji wa Kata yanayoratibiwa na Wizara ya Katiba na Sheria. “Sisi ndio tunaohusika kuwatambulisha wananchi, hii imekuwa ni changamoto kwetu sisi mpakani, mnapomtambulishi mtu kana kwamba yeye ana haki za uraia wa Tanzania tunawaomba kuwa wazalendo kweli” Kwa upande wake Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Adv. Dorice Dario amesema malengo ya kutoa elimu hiyo ni kuboresha utendaji kazi wa viongozi wa serikali za mitaa kwa kuzingatia haki za binadamu na utawala bora.

ASASI ZAIPONGEZA SERIKALI UTEKELEZAJI WA HAKI ZA BINADAMU NCHINI.

Image
  Mkurugenzi Msaidizi wa Haki za Binadamu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Beatrice Mpembo, akiongea kwenye Kikao Kazi  kujadili maendeleo ya utekelezaji wa mkataba  wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu pamoja na Itifaki ya Maputo. xxxxxxxxxxxxx Asasi za Kiraia na Haki za Binadamu zimeeleza kuridhishwa na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita katika kutekeleza Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu pamoja na Itifaki ya Maputo. Pongezi hizo zimetolewa wakati wa kikao kazi kilichofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Machi 19 hadi 21, 2025, ambapo wadau wamekutana na kujadili maendeleo ya utekelezaji wa mkataba huo. Akizungumza katika kikao hicho Wakili Laetitia Ntagazwa, Makamu wa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), amesema kuwa miongoni mwa mambo yanayosaidia katika kuimarisha Utawala wa Haki nchini ni pamoja na amani iliyopo jambo ambalo kila Mtanzania anapaswa kujivunia. Wakili Laetitia aliongezea kuwa licha ya Tanzania kumpoteza Kiongozi wa ...

OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA MWANZA YAHIMIZWA UWAJIBIKAJI

Image
 xxxxxxxxxxxxxxxx Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro Machi 18, 2025 Jijini Mwanza   ameongoza kikao na watumishi wa Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa   Mkoa huo ambapo amewahimiza umuhimu wa uwajibikaji katika kazi zao. Akizungumza katika   kikao hicho, Mhe. Ndumbaro amesisitiza kwamba ni muhimu kwa watumishi hao kuongeza ufanisi ili kuboresha huduma wanazotoa kwa wananchi na   kusaidia katika utoaji wa Haki kwa wananchi. Nae Mkuu wa Mashtaka wa Mkoa huo Bw. Joseph Mahugo, amemthibitishia Waziri Ndumbaro kwamba ofisi yake itaendelea kutoa huduma bora kwa maslahi ya taifa. Ziara ya Waziri Ndumbaro Jijini Mwanza ina lengo la kufanya ukaguzi wa shughuli za ofisi hiyo na kuona jinsi wanavyoweza kuboresha huduma zao kwa umma.

WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU ZINGATIENI SHERIA - KM MASWI

Image
  Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg.Eliakim Maswi akizungumza na wadau wa mashirika yasiyo ya kiserikali na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC)ambapo ametoa wito kwa wadau hao kuzingatia Sheria za Nchi na kufanya kazi kwa ushirikiano xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Ndg. Eliakim Maswi ametoa wito kwa mashirika yasiyo ya kiserikali pamoja na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) kuhakikisha wanafuata sheria za nchi, taratibu zilizowekwa, na kufanya kazi kwa ushirikiano bila ubinafsi. Maswi ametoa wito huo Machi 18, 2025 jijini Dodoma, wakati akifunga mafunzo ya siku mbili kwa wanachama wapya wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC.) Amesema kuwa mashirika hayo yana nafasi ya kutoa maoni na mapendekezo juu ya sheria zinazowasimamia, ili serikali iweze kufanya mabadiliko pale inapohitajika kwa ajili ya kuimarisha haki za binadamu kwa wananchi. Aidha, amewataka wanachama wapya wa THRDC kuwa mabalozi wa ha...

SIMAMIENI MALALAMIKO YA UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU - DKT. MWANDAMBO

Image
  Watendaji wa Jiji la Tanga wakiwa katika picha ya pamoja na wawezeshaji kutoka Wizara ya Katiba na Sheria mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya Uraia na Utawala Bora yaliyofanyika tarehe 15 Machi, 2025. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga Dkt. Stephen Mwandambo amewataka Watendaji wa Kata kusimamia malalamiko ya wananchi ya ukiukwaji wa Haki za Binadamu. Dkt. Mwandambo ameyasema hayo tarehe 15 Machi, 2025 wakati akifungua mafunzo ya Uraia na Utawala Bora kwa Kamati ya Usalama Wilaya, Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja  na Watendaji wa Kata wa Halmashauri ya Jiji la Tanga. “Mafunzo haya yatamsaidia Mkurugenzi kutoa nafuu kwenye utekelezaji wa  majukumu na tunategemea kuona  huduma zimeboreshwa katika ngazi zote baada ya mafunzo haya.“ Mwandambo amesema kupitia mafunzo waliyopata watatekeleza kwa vitendo na kuhakikisha falsafa ya “4R“ ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inasambaa kutoka katika ngazi za chini mpaka za juu za uong...

KAMATI ZA USALAMA ARUSHA ZATAKIWA KUFANYA KAZI KAMA TIMU

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda, akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Usalama Mkoa, Wawezeshaji   wa Mafunzo ya Utawala Bora na Urai mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya Uraia na Utawala Bora mafunzo   yanayoratibiwa na Wizara ya Katiba na Sheria kupitia Idara ya Katiba na Ufuatiliaji Haki. Tarehe 13 Machi, 2025. xxxxxxxxxxxxxxxxxxx Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. Paul Makonda, amewataka wajumbe wa Kamati za Usalama mkoani humo kufanya kazi kama timu, pamoja na kuwa na vipaumbele vya miradi ya kimkakati inayopaswa kujivunia kwa viongozi wa kitaifa wanapotembelea mkoa huo. Makonda amezungumza hayo wakati akifunga mafunzo ya elimu ya uraia na utawala bora kwa wajumbe wa Kamati ya Usalama wa Mkoa wa Arusha pamoja na kamati za usalama za Wilaya ya Arusha na Arumeru, yaliyoandaliwa na Wizara ya Katiba na Sheria, tarehe 13 Machi, 2025. Amesema Arusha kama mkoa unapaswa kuwa na mambo makubwa yanayoweza kufanywa kipaumbele kwa viongozi wa Kita...