Posts

VIONGOZI NA WATUMISHI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA WAWAPONGEZA WENZAO

Image
  Mkurugenzi wa Utajiri na Maliasilia Wizara ya Katiba na Sheria DCP Neema Mwanga akimkabidhi zawadi Bw. Alex Togo wakati wa hafla ya kuwapongeza watumishi waliopata watoto kati ya Januari hadi Machi, 2024. Tarehe 17 Aprili, 2024 Mtumba. Mkurugenzi wa Sera na Mipango Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Mbaraka Stambuli akimpongeza Bw. Judica Nkya wakati wa hafla ya kuwapongeza watumishi waliopata watoto kati ya Januari hadi Machi, 2024. Tarehe 17 Aprili, 2024 Mtumba. Mkurugenzi wa Sera na Mipango Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Mbaraka Stambuli akimkabidhi zawadi Bw. Eric Sezary wakati wa hafla ya kuwapongeza watumishi waliopata watoto kati ya Januari hadi Machi, 2024. Tarehe 17 Aprili, 2024 Mtumba. Baadhi ya Viongozi wa Wizara ya Katiba na Sheria kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi waliopewa zawadi kwa kupata watoto kati ya Januari hadi machi, 2024. Tarehe 17 Aprili, 2024 Mtumba. Viongozi na Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria kwenye hafla ya kuwapongeza watumishi wenzao wa

UJENZI WA MAHAKAMA ZA WILAYA NA ZA MWANZO UNAENDELEA – SAGINI

Image
  Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akijibu maswali Bungeni Dodoma tarehe 16 Aprili, 2024. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Na William Mabusi – WKS Dodoma Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini amesema Serikali inaendelea kutekeleza Mpango wa ujenzi na ukarabati wa majengo ya Mahakama kwa awamu kote nchini. Mhe. Sagini ameyasema hayo wakati akijibu swali kutoka kwa Mbunge wa Kalambo Mhe. Josephat Sinkamba Kandege Bungeni tarehe 16 Aprili, 2024 Jijini Dodoma. Katika swali lake la msingi lililoulizwa na Mhe. Rashid Shangazi kwa niaba yake, Mhe. Kandege alitaka kujua Serikali ina mpango gani wa kujenga na kukarabati Mahakama za Mwanzo Wilayani Kalambo. Katika kuweka msukumo wa ujenzi wa majengo ya Mahakama kote nchini Mhe. Sagini amesema ”Serikali ina Mpango wa ukarabati na ujenzi wa Mahakama kwa awamu. Kupitia Mpango huo katika mwaka wa fedha 2019/20 imeshajengwa Mahakama ya Mwanzo ya Msanzi katika jimbo la Kalambo. Pia katika mwaka wa fedha 2023/24 Mahakama

SAGINI AFURAHISHWA NA MAPOKEZI MoCLA

Image
  Naibu Waziri mpya wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akihutubia Watumishi wa Wizara hiyo alipopokelewa kwa mara ya kwanza Wizarani hapo, tarehe 08 Aprili, 2024 Ofisi za Wizara Mtumba Dodoma. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akimkaribisha Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini kuongea na Watumishi wa Wizara, tarehe 08 Aprili, 2024. Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akisalimiana na Watumishi wa Wizara baada ya kupokelewa Wizarani hapo, tarehe 08 Aprili, 2024. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akimkabidhi Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini ua alipopokelewa Wizarani hapo, tarehe 08 Aprili, 2024. Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akisalimiana na Watumishi wa Wizara baada ya kupokelewa Wizarani hapo, tarehe 08 Aprili, 2024. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akimkabidhi Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini vitendea kazi baada ya kupoke

UKATILI WOWOTE WANAOFANYIWA WATOTO UTOLEWE TAARIFA – DKT. CHANA

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akihutubia Kikao cha Tatu cha Jukwaa la Haki Mtoto, 05 Aprili, 2024 Jijini Arusha. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu akitoa salaam na kumkaribisha Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana kuhutubia Kikao cha Tatu cha Jukwaa la Haki Mtoto, 05 Aprili, 2024 Jijini Arusha. Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Msaada wa Kisheria Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Ester Msambazi akitoa wasilisho kwenye Kikao cha Tatu cha Jukwaa la Haki Mtoto, 05 Aprili, 2024 Jijini Arusha. Sehemu ya Washiriki kwenye Kikao cha Tatu cha Jukwaa la Haki Mtoto, wakisikiliza hotuba ya Mgeni Rasmi Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana. 05 Aprili, 2024 Jijini Arusha. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana kwenye picha ya pamoja na washirki wa Kikao cha Tatu cha Jukwaa la Haki Mtoto, kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Khatibu Kazungu. 05 Aprili, 2024 Jijini Aru

DKT. CHANA AMPOKEA JUMANNE SAGINI

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akimkabidhi ua la ukaribisho Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini alipowasili Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali mara baada ya hafla ya uapisho iliofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 04 Aprili, 2024. Anayeshuhudia katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bi. Mary Makondo. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akizungumza na viongozi wa Wizara na Taasisi zilizoko chini ya Wizara hiyo mara baada ya kumkaribisha na kumpokea Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Jumanne Sagini katika mapokezi yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali Jijini Dar es Salaam baada ya kuapishwa Ikulu, tarehe 04 Aprili, 2024. Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akizungumza na Viongozi wa Wizara na Taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo mara baada ya kuapishwa Ikulu Jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana. 04 Aprili, 2024. Katibu Mkuu wa W

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA MAJENGO YA MAHAKAMA

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana akijibu maswali Bungeni tarehe 02 Aprili, 2024 Jijini Dodoma. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Na William Mabusi – WKS Dodoma Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amesema Serikali inaendelea kuimarisha majengo ya Mahakama katika ngazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kujenga majengo mapya na kukarabati majengo chakavu. Dkt. Chana amesema hayo wakati akijibu maswali Bungeni leo tarehe 02 Aprili, 2024 Jijini Dodoma. ”Serikali kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania imeendelea kuimarisha majengo ya Mahakama katika ngazi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kujenga majengo mapya na kukarabati majengo chakavu kwa awamu kwa kuzingatia uwezo wa kibajeti.” Amesema Dkt. Chana akijibu swali la  Mhe. Francis Isack Mtinga Mbunge wa Wilaya ya Mkalama aliyetaka kujua ujenzi wa Mahakama kwenye Wilaya hiyo utaanza lini. Mhe. Waziri amesema Wilaya ya Mkalama ambayo ni moja ya Wilaya nne ambazo bado huduma za Mahakama zinapatikana kupitia Wila

KAMATI YAIPONGEZA SERIKALI UJENZI WA JENGO LA WAKILI MKUU WA SERIKALI

Image
  Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo akitoa maelezo ya awali ya maendeleo ya ujenzi wa jengo la Ofisi za Wakili Mkuu wa Serikali kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria tarehe 27 Machi, 2024 Mji wa Serikali Mtumba Dodoma. Kaimu Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Bw. Mark Mulwambo akitoa maelezo kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria tarehe 27 Machi, 2024 Mji wa Serikali Mtumba Dodoma. Mkandarasi wa mradi Eng. Baraka Mosha akitoa maelezo ya ujenzi wa jengo la Ofisi za Wakili Mkuu wa Serikali kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria tarehe 27 Machi, 2024 Mji wa Serikali Mtumba Dodoma. Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo, viongozi kutoka Wizarani na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kwenye picha ya pamoja na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria mbele ya jengo la Wakili Mkuu wa Serikali linalojengwa  Mji wa Serikali Mtumba Dodoma, tarehe 27 Machi, 2024. xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx