Posts

Showing posts from November, 2019

DPP afuta Kesi 59 zaidi jijini Mbeya

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Balozi Dkt Augustine Mahiga (Mb) katikati akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Mh. Chalya J. Nyangidu (wa pili kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Mashitaka Biswalo Mganga (wa pili kulia), walipotembelea Ofisi ya Mkuu huyo wa Wilaya leo tarehe 28 Nov. 2019 wakati wa ziara ya kikazi wilayani humo. Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Balozi Dkt Augustine Mahiga (Mb) akisalimiana na afisa wa magereza wakati wa ziara ya kikazi katika gereza la Tukuyu Wilaya ya Rungwe Jijini Mbeya. Kushoto ni Mkuu wa Gereza la Tukuyu ASP. Samwel J. Kaluwa akiwatambulisha Staff wa gereza hilo mbele ya Waziri. Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Balozi Dkt Augustine Mahiga (Mb) kulia akiwa na mwenyeji wake Kamishna Msaidizi wa Magereza Mkoa wa Mbeya Mathias   Mkama (ACP) katikati, alipotembelea Gereza Kuu la Ruanda Mbeya 27 Nov. 2019. Kushoto ni Kamishna Msaidizi   wa Magereza na Mkuu wa Gereza la Ruanda Mbeya Vendeline Tesha wakati wa ziara ya kikazi jiji

RAIA WA ETHIOPIA WALIOMALIZA VIFUNGO WARUDI NCHINI KWAO – WAZIRI MAHIGA

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga Ataka raia wa Ethiopia waliomaliza vifungo vyao warudishwe nchini kwao. Waziri Mahiga ameyasema hayo katika ziara yake ya kikazi ya siku saba katika Mikoa ya Iringa, Njombe na Mbeya ambapo anatembelea magereza ili kuona Haki Jinai inavyotekelezwa katika mikoa hiyo. “Hakuna sababu kwa nini raia hawa waendelee kutumia gharama kubwa ya Serikali yetu wakati wameshamaliza vifungo vyao, naahidi kuwa tutatumia kila njia kuhakikisha Serikali inatua mzigo huu”, alisema Balozi Mahiga. Akiwa ameambatana na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Ndg. Biswalo Mganga, Waziri Mahiga alianza ziara yake kwa kutembelea gereza la Wilaya ya Iringa mjini na kujionea namna Haki Jinai inavyotekelezwa katika gereza hilo. Waziri Mahiga alizipongeza taasisi za Haki Jinai Mkoani humo kwa kuendelea kushirikiana katika kuhakikisha haki jinai inatekelezwa ipasavyo na kuepuka vitendo vya rushwa, unyanyasaji na ubambikizaji wa kesi kwa watuhumiwa.

MAFANIKIO YA MIAKA MINNE YA SERIKALI YA AWAMU YA TANO KATIKA SEKTA YA SHERIA

Image
Kuanzishwa kwa Divisheni ya Mahakama Kuu ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi ni miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana katika Sekta ya Sheria ndani ya kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Tano.

MWENYEKITI TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA AMTEMBELEA WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA OFISINI KWAKE

Image
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora, Mheshimiwa Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu (kushoto) akimkabidhi Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Augustino Mahiga baadhi ya machapisho kutoka tume katika kikao kifupi kilichofanyika katika ofisi za Wizara ya Katiba na Sheria. Waziri wa Katiba na Sheria, Mh Mahiga akiongea na ujumbe waTume ya Haki za Binadamu na Utawala bora uliotembelea ofini kwake mapema Novemba 18, 2019. Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Augustino Mahiga (katikati) akiwa na Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora, Mheshimiwa Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu (kulia kwake). Wengine ni Makamishna wa Tume, kutoka kulia ni Mheshimiwa Amina Talib Ali, Mheshimiwa, Thomas Masanja, Mheshimiwa, Dkt. Fatma Rashid Khalfan na Makamu Mwenyekiti, Mohamed Khamis Hamad. Kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Profesa Sifuni Mchome, Mheshimiwa Khatib Mwinyi Chande na Mheshimiwa Nyanda Josiah Shuli

HABARI PICHA: WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA AKIPANDA MITI KATIKA ENEO LA WIZARA

Image
DODOMA: Katika juhudi za kumuunga Mkono Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan Dodoma kuwa ya kijani Waziri wa katiba na Sheria Dr. Balozi Agostino Mahiga kwa kushirikiana na Watumishi wa Wizara wamefanya zoezi la upandaji miti katika eneo la Wizara hiyo. Katibu Mkuu wa Katiba na Sheria {wa kwanza} Prof. Sifuni Mchome akimuongoza Waziri wa Katiba na Sheria kuelekea katika eneo lililoandaliwa kwa ajili ya upandaji miti Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma leo. Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Dkt Balozi Agostino Mahiga (Mb) {kushoto} akichagua miti kabla ya kuanza zoezi la upandaji miti katika maeneo ya Wizara  Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma leo. Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Dkt Balozi Agostino Mahiga (Mb) {katikati} akiandaa shimo kabla ya kupanda mti katika eneo la ofisi za Wizara  Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma. Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Dkt Balozi Agostino Mahiga (Mb) {katikati} akipanda mti katika eneo la ofisi za

Wizara ya Katiba Yaunga Mkono Kampeni ya Kuikijanisha Dodoma

Image
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Profesa Sifuni Mchome akizungumza na wafanyakazi wa wizara hiyo kabla ya kuanza zoezi la upandaji miti katika eneo la Ofisi za wizara hiyo zilizopo Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma leo. Zoezi hilo ni jitihada za Wizara hiyo katika kuunga mkono kampeni ya Makamu wa Rais ya kuifanya Dodoma inakuwa ya kijani.