DKT MAHIGA AWATAKA WATENDAJI WA SERIKALI KUSIMAMIA KIKAMILIFU ZOEZI LA USAJILI WA VIFO NCHINI

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika picha ya pamoja Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA na viongozi wa Mkoa wa Njombe baada ya kikao cha tathmini cha viongozi kuhusu mpango wa maboresho na usajili wa vifo katika Mkoa huo.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiongea na viongozi wa Mkoa wa Njombe kuhusu mpango wa Maboresho na usajili wa vifo katika Mkoa huo.
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini Bi. Emmy Hudson akiongea kwenye kikao cha tathmini cha viongozi wa Mkoa wa Njombe kuhusu mpango wa maboresho na usajili wa vifo Mkoani humo.


xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Dkt Mahiga awataka watendaji wa Serikali kusimamia kikamilifu usajili wa vifo nchini

Licha ya kuwepo kwa faida nyingi za usajili wa vifo nchini, lakini kumekuwepo na mwamko mdogo wa wananchi kuona umuhimu wa zoezi hilo mara baada ya kifo.

Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi yao, idadi ya vifo nchini  vilivyosajiliwa inaonesha ni asilimia 17.5% tu hii inamaanisha vifo vingi haviandikishwi nchini.

Katika tathmini ya zoezi la usajili wa vifo mkoa wa Njombe lililofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya mji wa Njombe, Waziri wa Katiba na Sheria Balozi Dkt. Augustine Mahiga amesema takwimu hizo haziridhishi na kuwataka watendaji kufanya jitihada za ziada ili kufikia malengo ya zoezi.

“Takwimu hizi haziridhishi kwa hiyo tufanye jitihada za maksudi ili tuweze kufikia asilimia kubwa zaidi na ninaomba mikoa mingine iige mfano wa Njombe kwasababu katika asilimia Njombe bado mnaongoza ukilinganisha na mikoa mingine” amesema Waziri Mahiga

Dkt. Mahiga aliongeza kuwa ni muhimu kuandikisha na kupata cheti cha kifo mara inapotokea ili kuweza kupata stahiki zinazomuhusu marehemu.

“Ni muhimu sana kuhakikisha tunaandikisha vifo ili kupata vyeti vya kifo ambavyo vinatumika kama uthibitisho wa kisheria na hutumiwa na familia na ndugu kupata stahiki mbali mbali zinazomuhusu marehemu. Ni muhimu kusajili vifo mara tu vinapotokea hata kama ni vya watoto waliozaliwa na kuishi kwa dakika chache” ameongeza Mahiga.

Kwa upande wake Kaimu Kabidhi Wasii Mkuu/Afisa Mtendaji Mkuu Bi Emmy Hudson amesema Utekelezaji wa mpango wa usajili wa matukio ya vifo katika Mkoa wa Njombe ninsehemu ya mageuzi makubwa yanayofanywa na Serikali kwa kushirikiana na wa maendeleo katika kuhakikisha kwamba kiwango cha usajili wa matukio muhimu ya binadamu (Civil Registration and Vital Statistics - CVRS) kinakuwa Bora zaidi kwani hali kwa sasa siyo nzuri.

Hii ni programu ya pili ya mkakati huu kutekelezwa katika Mkoa wa Njombe unaounganisha utekelezaji wa usajili wa watoto chini ya miaka mitano.

"Usajili wa kifo siyo jambo geni kwani umekuwa ukifanyika tangu wakati wa ukoloni japokuwa mpaka sasa mwitikio bado ni mdogo kutokana na sababu mbalimbali ikiwa pamoja na wananchi kutokuona umuhimu wake." Amesema Emmy Hudson.

"Kama wakala tunaendelea kuhamasisha wananchi na kusisitiza kwamba ni muhimu sana vifo vyote visajiliwe mara tu vinaootokea" ameongeza Emmy Hudson.

Viongozi wa Mkoa wa Njombe wamekutana leo tarehe 4 Desemba kufanya tathmini ya Mpango wa Maboresho ya Usajili wa Vifo katika Mkoa huo na kumhusisha Waziri wa Katiba na Sheria ambaye alikuwa katika ziara ya siku mbili kujionea utendaji kazi wa RITA.

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA