NAIBU KATIBU MKUU MPANJU ATOA WITO KWA VIONGOZI WA DINI KUHAMASISHA WANANCHI KUSAJILI WATOTO ILI KUPATIWA VYETI VYA KUZALIWA


xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju awaomba viongozi wa dini na kuwataka watendaji wa Serikali kuhamasisha waumini na wananchi waliopo maeneo yao kupeleka watoto kusajiliwa na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa.

Mpanju ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa mpango wa usajili wa watoto wa umri chini ya miaka mitano katika mikoa ya Morogoro na Pwani uliofanyika wiki hii katika viwanja vya uwanja wa ndege Mkoani Morogoro.

“Nitoe wito kwa viongozi wa dini zetu popote walipo kwenye mikoa ya Morogoro na Pwani, viongozi wa kijamii, wenyeviti wetu wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji waliochaguliwa hivi karibuni na watendaji kwa ngazi zote kuhakikisha mnahamasisha wananchi wetu kwenye mikoa hii wajitokeze katika kampeni inayoendelea kuwasajili watoto na kupatiwa cheti bure”alisema.

Aidha ndg Mpanju aliwaeleza viongozi hao kwamba zoezi hilo linagusa mtoto aliyezaliwa mwishoni mwa mwaka 2014 mpaka wanaozaliwa sasahivi hivyo, wawahamasishe wazazi na walezi wajitokeze kusajili watoto na kupata vyeti bure.

 Mpanju alisisitiza “Kwa hiyo nitoe rai kwa viongozi wa dini na watendaji wa Serikali kote nchini ambako kampeni hii inaendelea tutumie mimbali za makanisa, misikiti na majukwaa yetu ya kisiasa na kwenye maeneo ya kazi tuhakikishe habaki mtoto mwenye sifa bila kusajiliwa na kupata cheti”

Zoezi hili la uandikishaji linaloendelea katika mikoa 15 ya Tanzania Bara linatarajiwa kuifikia mikoa mingine yote iliyobaki ndani ya kipindi cha miaka mitatu kuanzia sasa.

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA