SIKU YA MAADILI NA HAKI ZA BINADAMU KUADHIMISHWA KITAIFA DESEMBA 11 MWAKA HUU.
Waziri wa Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuwafahamisha kuhusu maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yanayotarajiwa kufanyika Desemba 11, Jijini Dodoma. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju na Kulia ni Kamishna wa Maadili na Viongozi wa Umma Mhe. Jaji mstaafu Harold Nsekela.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju akiongea waandishi wa habari (hawapo pichani) kuwafahamisha kuhusu maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yanayotarajiwa kufanyika Desemba 11 Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe. Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu akiongea waandishi wa habari (hawapo pichani) kuwafahamisha kuhusu maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu.
Viongozi mbalimbali wakimsikiliza Waziri wa Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika wakati akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuwafahamisha kuhusu maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yanayotarajiwa kufanyika Desemba 11, Jijini Dodoma.
Sehemu ya waandishi wa habari waliohudhuria kikao na viongozi mbalimbali kufahamishwa kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Desemba 11, 2019.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju akiongea waandishi wa habari (hawapo pichani) kuwafahamisha kuhusu maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yanayotarajiwa kufanyika Desemba 11 Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe. Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu akiongea waandishi wa habari (hawapo pichani) kuwafahamisha kuhusu maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu.
Viongozi mbalimbali wakimsikiliza Waziri wa Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika wakati akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuwafahamisha kuhusu maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yanayotarajiwa kufanyika Desemba 11, Jijini Dodoma.
Sehemu ya waandishi wa habari waliohudhuria kikao na viongozi mbalimbali kufahamishwa kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Desemba 11, 2019.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
WAZIRI MKUCHIKA ATAKA WANANCHI WATEKELEZE WAJIBU WAO ILI KUPATA HAKI
ZAO
Wananchi wametakiwa kufahamu wajibu
wao katika kila eneo pale wanapodai haki zao ili kuwezesha haki hizo kupatikana
kwa wakati.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Ofisi
ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Uawala Bora Mhe. George Mkuchika
wakati akiongea na waandishi wa habari na kuufahamisha Umma kuhusu Maadhimisho
ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yanayotarajiwa kufanyika Disemba 11,
2019 Jijini Dodoma.
“Wanahabari, matarajio yangu ni
kwamba katika kuuhabarisha Umma, mtachambua haya ilimkila upande na hasa
mwananchi ambaye pamoja na kudai haki zake, afahamu pia wajibu wake katika kila
eneo” alisema.
Aliongeza ““Uadilifu unaanzia
ngazi ya familia ndipo Serikali itapata watumishi waadilifu wanaozingatia
misingi na kanuni za utumishi wa Umma”.
Waziri Mkuchika amesema
tunapoadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binadamu nchi inajitathmini namna
inavyozingatia maadili, kudhibiti rushwa na kufuata taratibu katika manunuzi na
nidhamu za watumishi zinavyosimamiwa.
Aidha, Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju alisema sheria za Utekelezwaji wa
Maadili na Haki za Binadamu zipo na zinafuatwa ipasavyo hivyo hali ya upatikanaji
wa haki za binadamu kwa sasa unaendelea vizuri.
Naye, Mwenyekiti wa Tume ya Haki
za Binadamu na Utawala Bora Mhe. Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu alisema Hali ya
utekelezwaji wa Haki za Binadamu nchini uko vizuri kwa sasa kwani haki hizo
zimekuwa zikitekelezwa kikamilifu katika sehemu mbalimbali ikiwemo Afya, Elimu
na Miundombinu.
Kauli Mbiu kwa mwaka huu ni “Utumishi
wa Umma ni Nguzo Muhimu katika Kuimarisha Utawala Bora na Haki za Binadamu”
Kongamano la kuhitimisha
Maadhimisho hayo linatarajiwa kufanyika Disemba 11 ma litahusisha watumishi
waandamizi wa Serrikali wakiwemo Makatibu Wakuu, Wakuu wa Taasisi na Mashirika
ya Serikali.
Comments
Post a Comment