SIKU YA MAADILI NA HAKI ZA BINADAMU KUADHIMISHWA KITAIFA DESEMBA 11 MWAKA HUU.

Waziri wa Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuwafahamisha kuhusu maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yanayotarajiwa kufanyika Desemba 11, Jijini Dodoma. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju na Kulia ni Kamishna wa Maadili na Viongozi wa Umma Mhe. Jaji mstaafu Harold Nsekela.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju akiongea waandishi wa habari (hawapo pichani) kuwafahamisha kuhusu maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yanayotarajiwa kufanyika Desemba 11 Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora  Mhe. Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu akiongea waandishi wa habari (hawapo pichani) kuwafahamisha kuhusu maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu.

Viongozi mbalimbali wakimsikiliza Waziri wa Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika wakati akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuwafahamisha kuhusu maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yanayotarajiwa kufanyika Desemba 11, Jijini Dodoma.

Sehemu ya waandishi wa habari waliohudhuria kikao na viongozi mbalimbali kufahamishwa kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Desemba 11, 2019.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
WAZIRI MKUCHIKA ATAKA WANANCHI WATEKELEZE WAJIBU WAO ILI KUPATA HAKI ZAO

Wananchi wametakiwa kufahamu wajibu wao katika kila eneo pale wanapodai haki zao ili kuwezesha haki hizo kupatikana kwa wakati.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Uawala Bora Mhe. George Mkuchika wakati akiongea na waandishi wa habari na kuufahamisha Umma kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yanayotarajiwa kufanyika Disemba 11, 2019 Jijini Dodoma.

“Wanahabari, matarajio yangu ni kwamba katika kuuhabarisha Umma, mtachambua haya ilimkila upande na hasa mwananchi ambaye pamoja na kudai haki zake, afahamu pia wajibu wake katika kila eneo” alisema.

Aliongeza ““Uadilifu unaanzia ngazi ya familia ndipo Serikali itapata watumishi waadilifu wanaozingatia misingi na kanuni za utumishi wa Umma”.

Waziri Mkuchika amesema tunapoadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binadamu nchi inajitathmini namna inavyozingatia maadili, kudhibiti rushwa na kufuata taratibu katika manunuzi na nidhamu za watumishi zinavyosimamiwa.

Aidha, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju alisema sheria za Utekelezwaji wa Maadili na Haki za Binadamu zipo na zinafuatwa ipasavyo hivyo hali ya upatikanaji wa haki za binadamu kwa sasa unaendelea vizuri.

Naye, Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe. Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu alisema Hali ya utekelezwaji wa Haki za Binadamu nchini uko vizuri kwa sasa kwani haki hizo zimekuwa zikitekelezwa kikamilifu katika sehemu mbalimbali ikiwemo Afya, Elimu na Miundombinu.

Kauli Mbiu kwa mwaka huu ni “Utumishi wa Umma ni Nguzo Muhimu katika Kuimarisha Utawala Bora na Haki za Binadamu”

Kongamano la kuhitimisha Maadhimisho hayo linatarajiwa kufanyika Disemba 11 ma litahusisha watumishi waandamizi wa Serrikali wakiwemo Makatibu Wakuu, Wakuu wa Taasisi na Mashirika ya Serikali.







Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA