WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA KUZINGATIA WELEDI WA TAALUMA ZAO



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika akifungua Kongamano la Kuadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binadamu, katika ukumbi wa Bunge wa Pius Msekwa jijini Dodoma.




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (katikati mstari wa mbele) na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa  (wa tatu kutoka kulia mstari wa mbele), Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe. Jaji Mathew Mwaimu (wa pili kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Taasisi za Umma, baada ya ufunguzi wa Kongamano la Kuadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binadamu katika ukumbi wa Bunge wa Pius Msekwa jijini Dodoma.


Baadhi ya viongozi wa Taasisi mbalimbali za Umma wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika  wakati akifungua Kongamano la Kuadhimisha Siku ya Maadili na Haki za Binadamu, katika ukumbi wa Bunge wa Pius Msekwa jijini Dodoma


XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX


Watumishi wa Umma wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia weledi wa taaluma zao.
kauli hiyo imetolewa   na Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kepteni Mstaafu George Mkuchika wakati akifungua maadhimisho ya siku ya maadili na haki za bianadamu kitaifa jijini Dodoma ambapo amewataka watumishi wa Umma kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia maadili.
“Tunaona Maadili ndio neno la Msingi Miongoni mwa jitihada za serikali ni kutunga sheria na kanuni mbalimbali zinazozingatia Maadili na Kanuni za utumishi wa umma, hivyo niwaase watumishi wa umma kuzingatia katika kufuata na kusimamia sheria  na Miongozo ya utumishi kwa lengo la kuboresha utawala bora” amesema.
Aidha, Waziri Mkuchika amesema suala la mfumo wa Mtandao limekuwa na mchango mkubwa katika kuhakiki watumishi feki pamoja na uadilifu wa matumizi ya fedha za umma.
Awali  akizungumza katika maadhimisho hayo, Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora  Mhe. Mary Mwanjelwa amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imejikita katika masuala ya uadilifu na uzalendo hivyo kila mmoja anapaswa kuepuke kufanya mambo yasiyofaa katika taifa.
Sisi tunatakiwa kuwa mfano bora katika kusimamia uadilifu na utawala bora hivyo niwaase watumishi wa umma kuwa jambo la uadilifu ni jambo la muhimu sana”
Kwa upande wake Kamishina wa Sekretarieti ya Maadili ya viongozi wa Umma Jaji Mstaafu Harold Nsekela ameelezea chimbuko la siku hiyo kuwa ni siku ya kimataifa ya kuzuia na kupambana na Rushwa ambayo huadhimishwa Desemba 09 ya kila mwaka
Tangu mwaka 2017 maadhimisho ya siku ya maadili na haki za bianadamu kitaifa yamekuwa yakifanyika Jijini Dodoma kufuatia maamuzi ya Serikali kuhamishia makao makuu jijini hapa na kauli mbiu kwa mwaka huu ni “Maadili katika Utumishi wa Umma ni Nguzo Muhimu katika Kuimarisha Utawala Bora na Haki za Binadamu”

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA