Posts

Showing posts from 2020

WANYONGE NI LAZIMA WALINDWE NA SHERIA-DKT MWIGULU

Image
 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akiongea na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Shinyanga alipofanya ziara ya kikazi mkoani humo. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akiongea na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Shinyanga (hawapo pichani)  alipofanya ziara ya kikazi mkoani humo. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. John Pombe Magufuli imejipambanua kuwalinda wanyonge hivyo anapojitokeza mtu yeyote kutaka kuwaumiza ni lazima ashughulikiwe kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.   Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ametoa angalizo hilo tarehe 15 Disemba 2020 wakati akizungumza kwenye kikao kazi na kamati ya ulinzi na usalama ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe Anamringi Macha akiwa katika ziara ya kikazi ya siku moja Mkoani Shinyanga.   Nchemba amekemea vikali wananchi wanaotaka kuijaribu serikali inayoongozwa na Mhe Rais Dkt

ONGEZENI NGUVU KATIKA KUSIMAMIA HAKI ZA WANANCHI - MHE. NCHEMBA

Image
 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Mwigulu Nchemba akiongea na watumishi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (hawapo pichani) alipofanya ziara katika ofisi ya Tume hiyo. Wengine pichani ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo  Mhe. Geoffrey Mizengo Pinda (kulia) na mwingine ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo Ndg. Amon Mpanju. Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe. Mathew Maimu (aliyesimama) akitoa taarifa ya utekelezaji kwa Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Mwigulu Nchemba alipotembelea ofisi za Tume hiyo. Baadhi ya watumishi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora wakimsikiliza Waziri wa Katiba na Sheria alipofanya ziara katika ofisi za Tume hiyo. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Mwigulu Nchemba aitaka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kuongeza nguvu katika kusimamia na kusikiliza malalamiko ya wananchi. Mhe. Nchemba ameyasema hayo alipofanya ziara ya kwanza ya kikazi katika Tume hiyo tangu alipoapishwa kushika wadhifa huo katika

MKUU WA MKOA WA TANGA ATAKA TAASISI ZA UTOAJI HAKI ZIBORESHWE ILI ZIWEZE KUTOA HAKI KWA WAKATI

  XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martin Shigella ataka taasisi za utoaji haki ziendelee kuboreshwa ili haki iweze kupatikana kwa wakati. Mhe. Shigella aliyasema hayo wakati akifungua mafunzo kwa kamati za usalama za mkoa na Wilaya, kamati za maadili ya Mahakimu na Kamati za Parole mkoani Tanga ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria. Mhe. Mkuu wa Mkoa aliwaambia viongozi hao kuwa wana dhamana kubwa ya kuhakikisha nchi ina utulivu, amani na usalama hivyo waitumie fursa hii ya kupata mafunzo hayo vizuri na kushirikishana na wengine. “Tuna dhamana kubwa ya kuhakikisha utulivu, usalama na amani ya nchi tunaitimiza kwa Pamoja, tutumie fursa hii vizuri na tushirikishane” alisema Mhe. Shigella. Aidha, Mkuu wa Mkoa amesema mamlaka za kutenda haki mkoani humo ikiwemo Mabaraza ya ardhi ya kata yamekuwa yakilalamikiwa sana kutokana na ufanisi wake ambao unasababishwa na watumishi wachache waliopo ambayo inasababisha ucheleweshwaji wa majukum

WAJUMBE WA MABARAZA YA ARDHI ACHENI KUPOKEA RUSHWA – MHE. NGUVIRA

  XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX   Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga Mhe. Toba Nguvira awaasa wajumbe wa mabaraza ya ardhi wilayani humo kuacha tabia ya kupokea rushwa na kunyima haki wananchi. Mhe. Nguvira aliyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya utawala bora, Wosia na Mirathi kwa watendaji kata na wenyeviti wa mabaraza ya ardhi wilayani humu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria ambayo kitaifa yalizinduliwa tarehe 12 Mkoani Tanga. Mkuu wa wilaya huyo aliwaambia watendaji kata na wenyeviti wa mabaraza ya kata hao wayatumie mafunzo hayo vizuri ili kumaliza migogoro mingi iliyopo ambayo inaanzia kwenye kata na inasababishwa na rushwa na hivyo kunyima haki baadhi ya wananchi. “Migogoro ya ardhi na mirathi ni mingi sana nchini na inasababishwa na rushwa” alisema Mkuu wa wilaya huyo. Aidha Mhe. Nguvira alisema sheria zimewekwa kuhakikisha haki inatendeke kwani kukosekana kwa haki kunapelekea machafuko katika jamii. Mhe. Nguvira aliwasisitiza wajumbe w

WATANZANIA TUWE NA UTAMADUNI WA KUANDIKA WOSIA KUEPUKA CHANGAMOTO ZA MIRATHI- JAJI MRUMA

  XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Tanga Mhe. Jaji Amir Mruma amesema watanzania tuwe na utamaduni wa kuandika wosia kwani suala la usimamizi wa mirathi huwa linakuwa rahisi sana pale kunapokuwa na wosia wa marehemu kuhusu mgawanyo wa mali zake pindi atakapoondoka duniani. “Mara nyingi wosia umekuwa ukirahisisha na kuondoa migogoro ya umiliki wa mali za marehemu na pia umekuwa ukibainisha nani atasimamia mali hizo kwa maendeleo ya familia husika” alisema Jaji Mruma. Jaji Mruma ameyasema hayo wakati akizindua rasmi Maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria yanayofanyika kitaifa Mkoani Tanga kuanzia tarehe 12 hadi 18 Novemba, 2020 yakilenga kupunguza changamoto za kisheria kwa wananchi. Mhe. Jaji Mruma alisema kwa utafiti walioufanya baada ya kukaa muda mrefu mahakamani wamegundua changamoto kubwa zaidi ya mirathi katika jamii inasababishwa na familia nyingi kutoandika wosia mapema kabla ya kufariki. Aliongeza kuwa usimamaizi

MAANDALIZI YA WIKI YA MSAADA WA KISHERIA YAANZA JIJINI TANGA

Image
  Kikao kazi cha maandalizi ya Wiki ya Msaada wa Kisheria chafanyika jijini Tanga na kufunguliwa na Katibu Tawala wa Mkoa Bi. Judica Omary.

WIZARA YA KATIBA KUSHIRIKIANA NA UNDP KUJENGA UELEWA KWA WANANCHI JUU YA UTAJIRI WA ASILI NA RASILIMALI ASILIA

Image
 Kikao kati ya Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) cha kujenga uelewa wa jukumu la Wizara kuhusiana na Uangalizi na Usimamizi waUtajiri wa Asili na Rasilimali za nchi chafanyika Wizarani hapo Mtumba, jijini Dodoma. Wataalam kutoka  Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)  wakifuatilia majadiliano wakati wa kikao chao na Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria. Mkurugenzi wa kitengo cha Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Rasilimali Asilia cha Wizara ya Katiba na Sheria  Bi Neema Mwanga akielezea jambo wakati wa kikao kati ya    Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP). Bi. Getrude kutoka kitengo cha mazingira UNDP akichangia mada. Mkurugenzi Idara ya Huduma za Kisheria kwa Umma Bw. Griffin Mwakapeje akichangia mada. Bw. Godfrey Mulisa kutoka UNDP akichangia mada. Picha ya pamoja ya Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria na wataalam kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja

KUMBUKUMBU YA MIAKA 21 YA KIFO CHA BABA WA TAIFA

Image
 

MAZUNGUMZO YA AMANI YATAJWA KUWA NJIA BORA NA SALAMA YA UTATUZI WA MIGOGORO NCHINI.

Image
  XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Mazungumzo ya amani ni muarobaini uliothibitika kutumika kama tiba ya migogoro ya ardhi Mvomero Mkoani Morogoro.   Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Albinus Mgonya wakati akitoa taarifa ya hali ya amani wilayani humo kwa Kamati ya Kitaifa ya Ujenzi wa Amani na Kuzuia Mauaji ya Kimbari iliyofika walayani kwake hivi karibuni.   Wakulima na wafugaji ni watanzania wanaoishi pamoja na kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kijamii, kisiasa na kiuchumi katika maeneo wanaoishi na zaidi, wengi wao ni wakulima na ni wafugaji kwa wakati mmoja hivyo njia ya mazungumzo ya amani imejipambanua kuwa tiba ya utatuzi wa migogoro inayowakabili.   "Unajua, hawa wakulima na wafugaji wanafahamiana kwasababu wanaishi pamoja, matumizi ya nguvu hususani vyombo vya ulinzi na usalama isingekuwa muarobaini, badala yake kwa kuwakutanisha na kuzungumza nao kumeonesha kuwa ni suluhisho la migogoro na ujenzi wa amani na utulivu baina yao.

PROF. MCHOME ATAKA WATANZANIA KUTUMIA VIZURI RASILIMALI ZILIZOPO NCHINI ILI KUJILETEA MAENDELEO

Image
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome akifungua kikao cha Makatibu Wakuu na Wakuu wa Taasisi cha kujadili Mfumo Jumuishi wa Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Rasilimali za Nchi kilichofanyika jijini Arusha. Washiriki wakichangia mada katika k ikao cha Makatibu Wakuu na Wakuu wa Taasisi cha kujadili Mfumo Jumuishi wa Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Rasilimali za Nchi.  Washiriki wakiendelea na kikao. Washiriki wa kikao wakiwa katika picha ya pamoja. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Nchi ya Tanzania imebarikiwa utajiri wa asili na rasilimali asilia ambazo zikitumika ipasavyo nchi na wananchi wake watakuwa na maendeleo ya kiuchumi. Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome wakati wa kikao cha Makatibu Wakuu na Wakuu wa Taasisi za Serikali waliokutana jijini Arusha kujadili Mfumo Jumuishi wa Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Rasilimali za nchi. Profesa Mchome alisema Sheria ya Usimamizi wa Utajiri wa Asili na Maliasilia i

MAADILI KWA WATUMISHI WA UMMA NI TIBA YA AMANI NCHINI

Image
 XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Usimamizi thabiti wa maadili kwa watumishi wa umma katika kata na vijiji mkoani Morogoro umetajwa kuwa sababu ya kupunguza migogoro kati ya wakulima na wafugaji.   Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Eng. Emmanuel N.M. Kalobelo alipotembelewa ofini kwake leo na Kamati ya Kitaifa ya Ujenzi wa Amani na Kuzuia Mauaji ya Kimbari.   Eng. Kalobelo amesema ukosefu wa maadili kwa watendaji wa kata na vijiji umeonekana kuwa kichocheo cha migogoro na uvunjifu wa amani katika maeneo mengi nchini lakini Serikali chini ya Mhe. Rais Dkt. John Joseph Pombe Magufuli imefanya kazi kubwa ya kulikomesha tatizo hilo mkoani Morogoro.   "Siku za nyuma Mkoa wa Morogoro ulikuwa kati ya mikoa yenye migogoro mingi ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji lakini baada ya kufanya utafiti wa kina tukagundua watendaji na viongozi wa kata na vijiji walikuwa ndiyo chanzo kwani waliidhinisha uuzaji wa maeneo yasiyopimwa bila kufuata taratibu sahihi.

WATUMISHI WIZARA YA KATIBA NA SHERIA WASISITIZWA KULINDA MALI ZA UMMA

Image
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome ambaye ni mwenyekiti wa baraza la wafanyakazi la wizara hiyo akiongoza mkutano huo katika ukumbi wa mikutano wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. Wajumbe wa baraza la wafanyakazi la Wizara ya Katiba na Sheria wakiendelea na mkutano huo. Zoezi la kuhesabu kura za uchaguzi wa Katibu wa baraza likiendelea. Katibu wa Baraza la wafanyakazi Wizara ya Katiba na Sheria Bi Basuta Milanzi (kushoto) akiwa na Katibu Msaidizi wa Baraza hilo Bw. Felix Chakila baada ya kuchaguliwa kushika nafasi hizo. Naibu Katibu Mkuu Ndg. Amon Mpanju akiwa amegusa kwa fimbo mchanga unaohama. Wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiwa mbele ya mchanga unaohama. Nyumbu ni moja ya wanyama ambao ni vivutio vilivyopo katika bonde la Ngorongoro. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wametakiwa kulinda mali za umma kama za kwao binafsi ili ziweze kudumu na kutumika kwa muda mrefu. Maelekezo hayo

KASI YA MAENDELEO YATAJWA KUWA KICHOCHEO CHA AMANI NCHINI

Image
  XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Kasi ya maendeleo yatajwa kuwa kichocheo cha amani nchini. Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Khalfan Haule alipotembelewa na Kamati ya Kitaifa ya Ujenzi wa Amani na Kuzuia Mauaji ya Kimbari ofisini kwake leo.   Dkt. Haule ametaja mafanikio yaliyofanywa na Rais wa Awamu ya Tano Mhe. Dkt. John Joseph Pombe Magufuli katika Sekta za Afya, Elimu, Barabara, Umeme, Maji na upatikanaji haki kwa wakati kuwa ni kichocheo cha ujenzi wa amani na utulivu hapa nchini.   "Huduma za jamii kama maji, elimu, umeme, afya, usafiri na usafirishaji ni haki ya msingi ya kila mwananchi. Naipongeza Serikali yangu chini ya Rais wetu mpendwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli kwa kuyapa kipaumbele masuala haya muhimu katika ujenzi wa amani na uchumi wa Taifa kwa kwa ujumla" amesema Dkt Haule.   Mwananchi akipata haki ya maendeleo kwa kuboreshewa na kusogezewa karibu huduma za jamii na nyingine hawezi kujihusisha na migogoro yo

WATAALAM WA SHERIA KUTOKA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA NA TAASISI NYINGINE WAJADILIANA KUHUSU MAREKEBISHO YA SURA YA 16

Image
Wataalam kutoka Wizara ya Katiba na Sheria na Wizara na Taasisi nyingine za Serikali wakiwa katika majadiliano ya mapitio ya sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16. wataalam hao walianza kupitia vifungu kimoja baada ya kingine vya sura ya 16 katika mafungu waliyogawana na sasa wanaendelea na majadiliano ya namna ya kuvirekebisha vifungu vilivyoonekana vinamapungufu na haviendani na wakati wa sasa. 

WADAU WA UJENZI WA AMANI WAMPONGEZA RAIS MAGUFULI

Image
  XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Wananchi wa Ngorongoro wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Joseph Magufuli kwa kujenga na kudumisha amani nchini.   Wameyasema hayo wakati wa Kikao na Kamati ya Kitaifa ya Ujenzi wa Amani na Kuzuia Mauaji ya Kimbari kilichofanyika leo katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, Mji mdogo wa Loliondo jijini Arusha.   Katika kikao hicho kilichohusisha viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, Wadau wa Amani ambao ni wakulima na wafugaji katika Wilaya hiyo pamoja na Wataalamu wa Kamati ya Kitaifa ya Amani kimelenga kubaini viashiria au vyanzo vya migogoro inayohusisha rasilimali na kusababisha uvunjifu wa amani ili kuitafutia suluhisho la kudumu kabla haijaleta madhara kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.   “Tunamshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa uongozi wake makini uliojaa busara na hekima na kuwezeha kuwa na amani katika jamii yetu. Siku hizi hatugombani na unaweza kuuza ng’o