Posts

Showing posts from January, 2020

KATIBU MKUU KATIBA NA SHERIA APOKEA UGENI WA MWAKILISHI MKAZI WA UNDP BI. CHRISTINE MUSISI

Image
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome (kulia) akiongea na Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Bi. Christine Musisi alipomtembelea ofisini kwake, Mji wa Serikali Mtumba, Jijini Dodoma kwa ajili ya kujitambulisha. Mwingine pichani ni  Bw. Godfrey Mulisa Mtaalam wa masuala ya utawala wa Umoja wa Mataiafa. Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome (kushoto) akiongea na Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa Bi. Christine Musisi (kulia) alipomtembelea ofisini kwake, Mji wa Serikali Mtumba, Jijini Dodoma kwa ajili ya kujitambulisha. Wengine pichani ni Wakurugenzi kutoka Wizarani hapo.

Habari Picha: Baraza la wafanyakazi Tume ya Kurekebisha Sheria

Image
 Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la TUMESHERIA na viongozi wao katika picha ya pamoja muda mchache kabla ya Uzinduzi wa Baraza hilo uliofanyika Ngorongoro Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome akiwahutubia Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la TUMESHERIA wakati wa  Uzinduzi wa Baraza hilo. Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome (katikati) akufuatilia mada katika Hafla ya Uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi la TUMESHERIA Afisa kutoka Ofisi ya Rais UTUMISHI Bi. Mwanvita Shamte (katikati) akitoa mada wakati wa Uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi TUMESHERIA Katibu wa TUGHE wa Mkoa wa Manyara Bw. Yakubu salim akifafanua jambo wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania.

Katibu MKuu Katiba na Sheria Awataka TUMESHERIA Kuendeleza Watumishi Kitaaluma

Image
Uongozi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania yatakiwa kuwaendeleza watumishi wake kitaaluma ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao na kuweka mpango maalum wa kutambua mchango wa watumishi wao katika maendeleo ya Tume na Taifa kwa ujumla. Maelekezo hayo yametolewa na Katibu Mkuu wa Katiba na Sheria Profesa Sifuni Mchome wakati akizindua Baraza jipya la Wafanyakazi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania katika Mkutano wa 14 wa Baraza hilo uliofanyika jana katika ukumbi wa Mikutano wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. “Watumishi ni rasilimali muhimu kuliko zote kwani ndiyo inayowezesha rasilimali nyingine ziwe na thamani, kwa maana hiyo kuna umuhimu mkubwa sana kwa Menejimenti ya Tume kuwawezesha   na kuwaendeleza watumishi wake kitaaluma kulingana na kada zao” alisema Prof. Mchome. Aidha, Prof. Mchome aliliasa Baraza la Wafanyakazi la TUMESHERIA kuweka mzingira mazuri yanayomruhusu mwajiri kuwajengea uwezo watumishi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kunakuw

WIZARA YA KATIBA NA SHERIA INAWATAKIA HERI YA MWAKA MPYA

Image