Posts

Showing posts from February, 2020

WIZARA YA KATIBA NA SHERIA WAFANYA UCHAGUZI KUPATA WAJUMBE WA BARAZA LA WAFANYAKAZI

Image
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Deogratias Yinza akiongoza kikao cha uchaguzi wa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo. Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dodoma Bw. Antelmas Tarimo (aliyesimama) akitoa sifa za wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi kabla ya uchaguzi wa wajumbe wa baraza hilo. Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakisikiliza maelekezo kabla ya kufanya uchaguzi wa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi. Msimamizi wa uchaguzi wa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Neema Dickson (kulia) akisimamia zoezi la kuhesabu kura. Msimamizi wa uchaguzi wa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Neema Dickson akitangaza matokeo ya uchaguzi huo. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Deogratias Yinza awataka wajumbe waliochaguliwa kuwawakilisha wenzao kwenye baraza la wafanyakazi kuh

TANZANIA NA CHAMA CHA UTAWALA WA SHERIA CHA KIMATAIFA CHA IRELAND KUKOMESHA UNYANYASAJI WA KIJINSIA

Image
Wanachama wa Chama cha Utawala wa Sheria cha Kimataifa cha Ireland wakiwa katika kikao na wataalam kutoka Wizara ya Katiba na sheria kwenye kikao chao kuangalia maeneo ambayo wanaweza kushirikiana ili kuiboresha sekta ya Sheria nchini. Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali za Asili Bibi neema Mwanga (kulia) kutoka Wizara ya Katiba na Sheria akisisitiza jambo kwenye kikao na wageni kutoka  Chama cha Utawala wa Sheria cha Kimataifa cha Ireland walipokuwa wakijadiliana maeneo ambayo wanaweza kushirikiana ili kuiboresha sekta ya Sheria nchini. Picha ya pamoja ya Wakurugenzi wa Wizara ya Katiba na sheria na wageni kutoka Chama cha Utawala wa Sheria cha Kimataifa cha Ireland baada ya kumaliza kikao chao. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Wizara ya Katiba na Sheria kwa kushirikiana na Chama cha Utawala wa Sheria cha Ireland wajipanga kukomesha unyanyasaji wa kijinsia na watoto nchini. Katika kikao kilichofanyika Wizarani hapo mapema leo Mtumba, jijini Dodoma, wataa

NAIBU KATIBU MKUU MPANJU ATAKA WALEMAVU KUFUATA SHERIA ZA NCHI

Image
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Watu wenye ulemavu watakiwa kufuata sheria na taratibu ili kuepuka migongano na vyombo vya sheria nchini Tanzania. Akizungumza katika mahojiano maalumu na kituo cha Televisheni cha TBC 1 ofisini kwake Mtumba, jijini Dododma Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju ambaye pia ni mlemavu wa macho aliwataka wananchi wenye ulemavu watii sheria za nchi ili kuepukana na mkono wa sheria kwani ulemavu haumpi mtu yeyote uhalali wa kuvunja sheria. “Taratibu na sheria za nchi lazima zifuatwe bila kujali ulemavu wa mwananchi na niwaombe wenzangu watambue kwamba ulemavu siyo tiketi ya kuvunja sheria” amesema   Mpanju.   Naibu Katibu Mkuu huyo alisisitiza kwamba kila mwananchi bila kujali hali yake ana wajibu wa kufuata na kutii sheria zilizowekwa na nchi, vinginevyo ataadhibiwa kama sheria invyoelekeza. “Kukiwa na tataizo ni vema wawafuate viongozi na kuzungumza nao ili waweze kutatua changamoto walizonazo na sio kufan

BALOZI MAHIGA AONGOZA KIKAO CHA WAKUU WA HAKI JINAI KUANGALIA HALI HALISI YA MABARAZA YA ARDHI

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Taasisi za Haki Jinai nchini (Collegium) baada ya kumaliza kikao chao cha kuangalia hali halisi ya Mabaraza ya Ardhi nchini. Mjumbe wa kikao cha kuangalia hali halisi ya Mabaraza ya Ardhi nchini ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi kutoka TAMISEMI Bw. Stanley Kamana akifafanua jambo katika kikao hicho. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiongoza kikao cha Wakuu wa Taasisi za Haki Jinai nchini (Collegium) cha kuangalia hali halisi ya Mabaraza ya Ardhi nchini.

SERIKALI YAKABIDHIWA MALI ZENYE THAMANI YA ZAIDI TSH. BILIONI 58

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Balozi Augustine Mahiga akizungumza katika hafla ya Serikali kukabidhiwa mali zilizotaifishwa zenye thamani ya shilingi Bilioni 58. Wengine pichani , kushoto ni Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango na kulia ni Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko  Baadhi ya vipande vya dhahabu vikiwa katika begi. Makasha yaliyohifadhi mali zilizotaifishwa zikiwemo fedha na dhahabu. Baadhi ya Fedha zilizotaifishwa Mkurugenzi wa Mashtaka akiwaonesha viongozi baadhi ya magari yaliyotaifishwa. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX SERIKALI kupitia Ofisi ya Taifa ya Mashtaka chini ya uongozi wa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) imefanikiwa kupata amri za kutaifisha mali mbalimbali zinazohusiana na uhalifu sambamba na fedha zilizolipwa   kutokana na kesi za madini zilizopo katika akaunti ya AFR katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) zenye thamani ya zaidi ya Tsh Bilioni 58. Akizungumza na waandishi wa vyombo vya habar

MAKAMU MWENYEKITI TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWLA BORA ATEMBELEA BANDA LA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA KATIKA MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA

Image
Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mohamed Hamad akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Idara ya Uangalizi wa Utajiri na Rasilimali Asilia kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Neema Mwanga alipotembelea banda hilo kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Sheria. Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mohamed Hamad akipokea Katiba ya mwaka 1977 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka kwa Mkurugenzi wa Idara ya Uangalizi wa Utajiri na Rasilimali Asilia kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Neema Mwanga alipotembelea banda hilo kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Sheria.

NAIBU MWANASHERIA MKUU ATEMBELEA BANDA LA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

Image
Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Evaristo Longopa akiangalia baadhi ya vipeperushi vinavyogawiwa kwa wananchi wanaotembelea banda la Wizara ya Katiba na Sheria katika maadhimisho ya Wiki ya sheria yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.

NAIBU WAKILI MKUU WA SERIKALI ATEMBELEA BANDA LA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

Image
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Mhe. Gabriel Malata akifafanua jambo alipotembelea banda la Wizara ya Katiba na Sheria katika Maadhimisho ya Wiki ya Sheria yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma. Anayemsikiliza ni Mkurugenzi wa Idara ya Uangalizi wa utajiri na Rasilimali asilia wizarani hapo. Mkurugenzi wa Idara ya Uangalizi wa Utajiri na Rasilimali Asilia waWizara ya Katiba na Sheria Kamishna Neema Mwanga akifafanua jambo kwa Naibu Wakili wa Serikali Mhe. Gabriel Malata alipotembelea banda hilo katika maadimisho ya Wiki ya Sheria yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.

SPIKA NDUGAI ATEMBELEA BANDA LA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA KWENYE MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA

Image
Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Job Ndugai akipata maelezo kuhusu shughuli zinazofanywa na Wizara ya Katiba na Sheria alipotembelea banda la Wizara hiyo katika Maadhimisho ya Wiki ya Sheria yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma. Maafisa kutoka Wizara ya Katiba na Sheria wakimsikiliza Mhe. Ndugai alipotembelea banda la Wizara hiyo kutoka kulia ni Kamishna Neema Mwanga Mkurugenzi wa Idara ya Uangalizi wa utajiri wa asili na rasilimali asilia  katikati ni Bi. Ester Msambazi Wakili wa Serikali na mwingine ni Hussein Mandali Wakili. Vipeperushi mbalimbali kwa ajili ya kutoa elimu kwa Umma kwenye maadhimisho hayo.