NAIBU KATIBU MKUU MPANJU ATAKA WALEMAVU KUFUATA SHERIA ZA NCHI



XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Watu wenye ulemavu watakiwa kufuata sheria na taratibu ili kuepuka migongano na vyombo vya sheria nchini Tanzania.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na kituo cha Televisheni cha TBC 1 ofisini kwake Mtumba, jijini Dododma Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju ambaye pia ni mlemavu wa macho aliwataka wananchi wenye ulemavu watii sheria za nchi ili kuepukana na mkono wa sheria kwani ulemavu haumpi mtu yeyote uhalali wa kuvunja sheria.

“Taratibu na sheria za nchi lazima zifuatwe bila kujali ulemavu wa mwananchi na niwaombe wenzangu watambue kwamba ulemavu siyo tiketi ya kuvunja sheria” amesema  Mpanju. 

Naibu Katibu Mkuu huyo alisisitiza kwamba kila mwananchi bila kujali hali yake ana wajibu wa kufuata na kutii sheria zilizowekwa na nchi, vinginevyo ataadhibiwa kama sheria invyoelekeza. “Kukiwa na tataizo ni vema wawafuate viongozi na kuzungumza nao ili waweze kutatua changamoto walizonazo na sio kufanya vurugu kwa mwanvuli wa ulemavu au hali zao.”  Alisisitiza Mpanju.

Aidha, ndugu Mpanju aliwataka watu wenye ulemavu kutobweteka na badala yake wafanye kazi halali na kwa bidii ili kujipatia kipato kwani ulemavu haumpi mtu hela wala kutatua changamoto zozote za kimaisha.

“Ulemavu haukupi hela au maisha, hivyo ulemavu sio sababu ya kubweteka, watu wenye ulemavu wajielewe na kufanya kazi halali ili kujiongezea kipato” Alisema.

Vilevile alisisitiza kuwa watu wenye ulemavu ni jukumu lao kusimamia mambo yao wenyewe ikiwemo ujenzi wa majengo yanayofaa, kwa mfano, Sheria namba 9 ya mwaka 2010 ya watu wenye ulemavu imeelekeza majengo yote mapya yanayojengwa yazingatie miundombinu rafiki kwa walemavu. Hivyo, watu wenye ulemavu wajitahidi kutafuta elimu, ajira, matibabu na mahitaji mengine muhimu wanayohitaji na sio kubakia wanyonge kwa kuona wananyanyaswa na kwamba hawapewi haki zao.

Wizara ya Katiba na Sheria inasimamia mfumo wa haki kupitia taasisi zilizo chini yake zinazochangia uwepo wa utawala wa sheria nchini. Wananchi wote wakiwemo watu wenye ulemavu watumie taasisi zote zilizo chini ya Wizara kuhakikisha wanapata haki zao.



Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA