TANZANIA NA CHAMA CHA UTAWALA WA SHERIA CHA KIMATAIFA CHA IRELAND KUKOMESHA UNYANYASAJI WA KIJINSIA

Wanachama wa Chama cha Utawala wa Sheria cha Kimataifa cha Ireland wakiwa katika kikao na wataalam kutoka Wizara ya Katiba na sheria kwenye kikao chao kuangalia maeneo ambayo wanaweza kushirikiana ili kuiboresha sekta ya Sheria nchini.

Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali za Asili Bibi neema Mwanga (kulia) kutoka Wizara ya Katiba na Sheria akisisitiza jambo kwenye kikao na wageni kutoka  Chama cha Utawala wa Sheria cha Kimataifa cha Ireland walipokuwa wakijadiliana maeneo ambayo wanaweza kushirikiana ili kuiboresha sekta ya Sheria nchini.
Picha ya pamoja ya Wakurugenzi wa Wizara ya Katiba na sheria na wageni kutoka Chama cha Utawala wa Sheria cha Kimataifa cha Ireland baada ya kumaliza kikao chao.

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Wizara ya Katiba na Sheria kwa kushirikiana na Chama cha Utawala wa Sheria cha Ireland wajipanga kukomesha unyanyasaji wa kijinsia na watoto nchini.

Katika kikao kilichofanyika Wizarani hapo mapema leo Mtumba, jijini Dodoma, wataalam kutoka Chama cha Utawala wa Sheria cha Ireland wameahidi kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Katiba na Sheria na Taasisi zake ikiwemo Mahakama katika kuzuia unyanyasaji wa kijinsia na watoto kwani ni tatizo linaloonekana kushika kasi kwa sasa.

Akizungumza katika kikao kutazama maeneo ya ushirikiano baina ya Taasisi hizi mbili Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Kisheria kwa Umma Bw. Griffin Mwakapeje alisema ili kuleta matokeo chanya katika sekta ya sheria kwa sasa Tanzania inahitaji kushirikiana na wadau mbalimbali katika maeneo muhimu ikiwemo kuzuia unyanyasaji wa aina mbalimbali na kuwajengea uwezo watumishi kama Mawakili, Makarani na Mahakimu ili kuwawezesha kusimamia haki nchini.

Aidha, Bw. Griffin aliongeza kuwa wanawake wanaofanya shughuli za uchimbaji wa madini wanakumbana na changamoto nyingi kwani huko kuna unyanyasaji wa aina mbalimbali ikiwepo wa kijinsia hivyo ni muhimu jamii ielimishwe namna ya kulinda na kutetea haki zao ili waweze kufaidika na rasilimali za asili.

Chama cha Utawala wa Sheria cha Ireland kimekuwa kikitoa mchango mkubwa katika upatikanaji wa haki kwenye nchi mbalimbali za Afrika ikiwemo Tanzania.

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA