TANZANIA NA CHAMA CHA UTAWALA WA SHERIA CHA KIMATAIFA CHA IRELAND KUKOMESHA UNYANYASAJI WA KIJINSIA
Wanachama wa Chama cha Utawala wa Sheria cha Kimataifa cha Ireland wakiwa katika kikao na wataalam kutoka Wizara ya Katiba na sheria kwenye kikao chao kuangalia maeneo ambayo wanaweza kushirikiana ili kuiboresha sekta ya Sheria nchini.
Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali za Asili Bibi neema Mwanga (kulia) kutoka Wizara ya Katiba na Sheria akisisitiza jambo kwenye kikao na wageni kutoka Chama cha Utawala wa Sheria cha Kimataifa cha Ireland walipokuwa wakijadiliana maeneo ambayo wanaweza kushirikiana ili kuiboresha sekta ya Sheria nchini.
Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali za Asili Bibi neema Mwanga (kulia) kutoka Wizara ya Katiba na Sheria akisisitiza jambo kwenye kikao na wageni kutoka Chama cha Utawala wa Sheria cha Kimataifa cha Ireland walipokuwa wakijadiliana maeneo ambayo wanaweza kushirikiana ili kuiboresha sekta ya Sheria nchini.
Picha ya pamoja ya Wakurugenzi wa Wizara ya Katiba na sheria na wageni kutoka Chama cha Utawala wa Sheria cha Kimataifa cha Ireland baada ya kumaliza kikao chao.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Wizara ya Katiba na Sheria kwa
kushirikiana na Chama cha Utawala wa Sheria cha Ireland wajipanga kukomesha
unyanyasaji wa kijinsia na watoto nchini.
Katika kikao kilichofanyika
Wizarani hapo mapema leo Mtumba, jijini Dodoma, wataalam kutoka Chama
cha Utawala wa Sheria cha Ireland wameahidi kushirikiana kwa karibu na Wizara
ya Katiba na Sheria na Taasisi zake ikiwemo Mahakama katika kuzuia unyanyasaji
wa kijinsia na watoto kwani ni tatizo linaloonekana kushika kasi kwa sasa.
Akizungumza katika kikao kutazama
maeneo ya ushirikiano baina ya Taasisi hizi mbili Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya
Huduma za Kisheria kwa Umma Bw. Griffin Mwakapeje alisema ili kuleta matokeo
chanya katika sekta ya sheria kwa sasa Tanzania inahitaji kushirikiana na wadau
mbalimbali katika maeneo muhimu ikiwemo kuzuia unyanyasaji wa aina mbalimbali
na kuwajengea uwezo watumishi kama Mawakili, Makarani na Mahakimu ili
kuwawezesha kusimamia haki nchini.
Aidha, Bw. Griffin aliongeza kuwa
wanawake wanaofanya shughuli za uchimbaji wa madini wanakumbana na changamoto
nyingi kwani huko kuna unyanyasaji wa aina mbalimbali ikiwepo wa kijinsia hivyo
ni muhimu jamii ielimishwe namna ya kulinda na kutetea haki zao ili waweze
kufaidika na rasilimali za asili.
Chama cha Utawala wa Sheria cha
Ireland kimekuwa kikitoa mchango mkubwa katika upatikanaji wa haki kwenye nchi
mbalimbali za Afrika ikiwemo Tanzania.
Comments
Post a Comment