Posts

Showing posts from March, 2020

OFISI ZA KATA KUTUMIKA KUSAJILI WATOTO CHINI YA UMRI WA MIAKA MITANO

Image
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Amon Mpanju akitoa elimu ya namna ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa Korona kwa wananchi waliofika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma kusajili wa watoto walio chini ya Miaka Mitano unaofanywa na RITA. Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Amon Mpanju akishuhudia zoezi la usajili wa watoto chini ya umri wa miaka mitano katika kituo cha usajili kilichopo katika Hospitali ya Misheni Peramiho Mkoa wa Ruvuma. Baadhi ya Wazazi wakionesha vyeti vya kuzaliwa vya watoto wao walivyokabidhiwa na Naibu Katibu MKuu wa Katiba na Sheria Bw. Amon Mpanju baada ya kufanikiwa kuwasajili watoto wao. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini RITA umefanya maboresho ya mfumo wa usajili kuwezesha Vituo vya Afya pamoja ofisi za kata vitumike kuwasajili watoto na kupatiwa cheti cha kuzaliwa. Hayo yameelezwa jana na Msajili wa Vizazi na Vifo na Mratibu wa zoezi la U

WATUMISHI WIZARA YA KATIBA NA SHERIA WAPATA ELIMU NAMNA YA KUJIKINGA NA VIRUSI VYA CORONA

Image
Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiwasikiliza wataalam wa afya kutoka General hospital Mkoani Dodoma (hawapo pichani), walipofika kuwapa elimu kuhusu ugonjwa wa Corona. Wataalam hao waliwaeleza namna ugonjwa huo unavyoenezwa, jinsi ya kujikinga na hatua za kuchukua pale wanapomhisi mtu ameambukizwa virusi vya Corona. Daktari Elam Lazaru Yango kutoka General Hospital Mkoani Dodoma (aliyesimama) akitoa elimu kuhusu virusi vya Corona kwa watumishi wa Wizara ya Katiba na sheria.  Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiuliza swali kwa wataalam wa afya kutoka General Hospital Mkoani Dodoma wakati wakitoa elimu kuhusu virusi vya Corona kwa watumishi wa Wizara ya Katiba na sheria. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju (mwenye miwani nyeusi) akiuliza swali kwa wataalam wa afya kutoka General Hospital Mkoani Dodoma wakati wakitoa elimu kuhusu virusi vya Corona kwa watumishi wa Wizara ya Katiba na sheria.

MAFUNZO YA SHERIA NCHINI YAENDANE NA KASI YA UCHUMI WA VIWANDA

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Mh Balozi Dkt Augustine Mahiga (pili kulia) akisalimiana na Makamu Mkuu (Taaluma)  wa chuo kikuu cha Tumaini Makumira Prof. Mbise katika ziara ya kutembelea vyuo vya sheria nchini. Waziri wa Katiba na Sheria Mh Balozi Dkt Augustine Mahiga (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa chuo kikuu cha Mzumbe katika ziara ya kutembelea vyuo vya sheria nchini. Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof Sifuni Mchome (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa chuo kikuu cha Iringa katika ziara ya kutembelea vyuo vinavyofundisha sheria nchini. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Vyuo vinavyotoa elimu ya Sheria nchini vimeshauriwa kutengeneza mitaala ya mafunzo ya sheria inayoendana na kasi ya maendeleo ya kiuchumi na viwanda yanayofanywa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sasa ili kuongeza tija kiusimamizi na ulinzi wa miundombinu na maendeleo hayo kwa ustawi wa taifa na wananchi wake. Hayo yam

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA KAZI YA UJENZI WA MAHAKAMA NCHINI

Image
Baadhi ya Mafundi wakiendelea na ujenzi wa jengo la ghorofa nne la Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ambalo pia litatumika kama kituo jumuishi cha utoaji haki. Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria wakipokea maelezo kuhusu kukamilika kwa ujenzi wa jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi-Manyara.  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akizungumza jambo na Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Mhe. Emmanuel Mwakasaka wakati wa ziara ya Kamati hiyo ya kukagua ujenzi wa jengo la Mahakama Kuu Kanda ya Arusha. Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria wakikagua samani katika moja ya chumba cha Mahakama ya Wilaya ya Longido jijini Arusha. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria iliyoshirikisha viongozi wa juu wa Wizara ya Katiba na Sheria na Mahakama wamefanya ziara ya ukaguzi wa majengo yanayojengwa na Mahakama ya Tanzan