MAFUNZO YA SHERIA NCHINI YAENDANE NA KASI YA UCHUMI WA VIWANDA
Waziri wa Katiba na Sheria Mh Balozi Dkt Augustine Mahiga (pili kulia) akisalimiana na Makamu Mkuu (Taaluma) wa chuo kikuu cha Tumaini Makumira Prof. Mbise katika ziara ya kutembelea vyuo vya sheria nchini.
Waziri wa Katiba na Sheria Mh Balozi Dkt Augustine Mahiga (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa chuo kikuu cha Mzumbe katika ziara ya kutembelea vyuo vya sheria nchini.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof Sifuni Mchome (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa chuo kikuu cha Iringa katika ziara ya kutembelea vyuo vinavyofundisha sheria nchini.
Waziri wa Katiba na Sheria Mh Balozi Dkt Augustine Mahiga (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa chuo kikuu cha Mzumbe katika ziara ya kutembelea vyuo vya sheria nchini.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof Sifuni Mchome (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa chuo kikuu cha Iringa katika ziara ya kutembelea vyuo vinavyofundisha sheria nchini.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Vyuo
vinavyotoa elimu ya Sheria nchini vimeshauriwa kutengeneza mitaala ya mafunzo
ya sheria inayoendana na kasi ya maendeleo ya kiuchumi na viwanda yanayofanywa
na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sasa ili kuongeza tija kiusimamizi
na ulinzi wa miundombinu na maendeleo hayo kwa ustawi wa taifa na wananchi wake.
Hayo
yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome
katika ziara ya siku tatu ya kutembelea vyuo vya elimu ya juu vinavyofundisha
Sheria inchini ambapo alitembelea Chuo Kikuu cha Iringa na Chuo Kikuu Katoliki cha
Ruaha (Iringa), Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira (Arusha) pamoja na Chuo Kikuu Mzumbe,
Chuo Kikuu Kishiriki cha Jordani na Chuo Kikuu cha Waislam vyote vya Morogoro.
Katika
ziara hiyo Prof. Mchome alisema Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi
shupavu wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Joseph
Pombe Magufuli, imefanya mageuzi ya kimaendeleo kwa kutekeleza miradi mikubwa
inayochochea ukuaji wa uchumi nchini na yenye manufaa kwa wananchi akitolea
mfano wa ujenzi unaoendelea wa Reli ya Kisasa (SGR) na Bwawa la Umeme la Julius
Nyerere (JNHPP). Ni lazima elimu ya Sheria nchini ilenge kuwajenga wanasheria
nchini katika muktadha wa kushiriki kulinda na kusimamia miundombinu
inayojengwa na itakayojengwa ili kuleta tija maridhawa katika kuelekea uchumi wa
kati na uchumi wa viwanda kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.
“Hatuwezi
kuendelea kufundisha sheria za makosa ya jinai (criminal law) pekee kana kwamba
nchi hii ni ya wahalifu tu wakati ukweli uko wazi kuwa Serikali inatekeleza
miradi mikubwa katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu, nishati,
usafilishaji na uchukuzi kwa lengo la kuipeleka nchi kwenye chumi wa kati na wa
viwanda. Lazima tubadilike sasa kwa kuwapika wataalamu wetu wa Sheria ili
kushiriki katika kulinda na kusimamia miundombinu hii kisheria ikiwemo uandishi
wa mikataba.”
Nae
Kaimu Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Sheria kwa vitendo maarufu kama ‘Law School’
Dkt. Zakayo Lukumayi baada ya kuwasilisha mada iliyohusu maendeleo ya taaluma
ya sheria nchini amesema kwamba wameamua kushiriki katika ziara ya kuvitembelea
vyuo vinavyofundisha sheria kwaajili ya kutoa mrejesho wa hali ya taaluma ya sheria
nchini kutokana na uzoefu wa kuwafundisha wanasheria wanaopita katika chuo
hicho ili kwa pamoja waimarishe mfumo wa kufundisha wanasheria kwa lengo la
kupata wataalamu bora wa sheria nchini kwa maslahi ya Taifa.
“Tumeona
tutoe mrejesho wa hali halisi ya maendeleo ya taaluma ya sheria nchini kwa sasa
ili tujue wapi tulipotoka, na tulipo ili tushauriane namna ya kuboresha mitaala
yetu kwa lengo la kuendana na hali halisi ya mwelekeo wa nchi yetu kiuchumi.
Tunataka tuwe washindani katika sekta zote za kimkakati ili kuunga mkono
jitihada zinazofanywa na Rais wetu wa Awamu ya Tano, Dkt. Magufuli”. Alisisitiza
Dkt. Lukumay.
Kwa
upande wake Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Augustine
Mahiga aliyeambatana Katibu Mkuu Prof. Mchome, Naibu Katibu Mkuu, Bw. Amon
Mpanju, Kaimu Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Sheria ‘Law School’ Dkt. Zakayo
Lukumay pamoja na Mjumbe wa Baraza la Sheria nchini Dkt. Erasmo Nyika pamoja na
pongezi aliwaeleza viongozi na wanafunzi wa vyuo hivyo kuwa nchi yoyote duniani
haiwezi kupiga hatua kimaendeleo bila kuwa na sheria madhubuti zinazotungwa na kusimamiwa
na wanasheria waliopikwa vizuri kuendana na wakati na mwelekeo wa taifa husika
kiuchumi na kutenda haki kwa wakati, hivyo kuna haja kwa Taifa la Tanzania
kuzalisha wanasheria watakaokidhi mahitaji ya sheria nchini sambamba na kasi ya
maendeleo inayofanywa na Mhe Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
Comments
Post a Comment