WATUMISHI WIZARA YA KATIBA NA SHERIA WAPATA ELIMU NAMNA YA KUJIKINGA NA VIRUSI VYA CORONA

Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiwasikiliza wataalam wa afya kutoka General hospital Mkoani Dodoma (hawapo pichani), walipofika kuwapa elimu kuhusu ugonjwa wa Corona. Wataalam hao waliwaeleza namna ugonjwa huo unavyoenezwa, jinsi ya kujikinga na hatua za kuchukua pale wanapomhisi mtu ameambukizwa virusi vya Corona.

Daktari Elam Lazaru Yango kutoka General Hospital Mkoani Dodoma (aliyesimama) akitoa elimu kuhusu virusi vya Corona kwa watumishi wa Wizara ya Katiba na sheria. 

Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiuliza swali kwa wataalam wa afya kutoka General Hospital Mkoani Dodoma wakati wakitoa elimu kuhusu virusi vya Corona kwa watumishi wa Wizara ya Katiba na sheria.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju (mwenye miwani nyeusi) akiuliza swali kwa wataalam wa afya kutoka General Hospital Mkoani Dodoma wakati wakitoa elimu kuhusu virusi vya Corona kwa watumishi wa Wizara ya Katiba na sheria.

Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA