Posts

Showing posts from April, 2020

NAFASI ZA KAZI

Image

UTEKELEZWAJI WA RIPOTI YA MFUMO WA UTATUZI WA MIGOGORO YA ARDHI WATAKIWA KUKAMILIKA MAPEMA

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (katikati) akipokea ripoti ya mfumo wa utatuzi wa migogoro ya ardhi kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Mhe. Jaji Mstaafu Januari Msoffe (kulia) wakati wa makabidhiano hayo katika ofisi za Wizara hiyo, Mtumba, jijini Dodoma. Mwingine pichani ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Ndg. Casmir Kyuki.  Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Mhe. Jaji Mstaafu Januari Msoffe (aliyesimama) akifafanua jambo mbele ya Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga wakati wa makabidhiano ya ripoti ya mfumo wa utatuzi wa migogoro ya ardhi.  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania baada ya makabidhiano ya ripoti ya mfumo wa utatuzi wa migogoro ya ardhi. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Utekelezwaji wa ripoti ya mfumo wa utatuzi wa migogoro ya a

WIZARA YA KATIBA YAENDELEA KUIKIJANISHA DODOMA

Image
Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Utawala wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Edith Simtengu akipanda mti katika zoezi la upandaji miti katika viwanja vya Wizara hiyo Mtumba, Jijini Dodoma.. Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiendelea na zoezi la kukijanisha Dodoma kwa kupanda miti katika viwanja vya wizara hiyo. Bi Joyce Mtuma (kushoto) na Bi. Agnes Mkawe ambao ni watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiwa wamebeba mti kuupeleka kwenye shimo la kuupanda katika zoezi la upandaji miti lililofanyika leo (3/4/2020) katika viwanja vya wizara hiyo.

WATUMISHI WIZARA YA KATIBA WAPATA ELIMU YA KUJIKINGA NA VIRUSI VYA COVID19

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Dkt. Balozi Augustine Mahiga akifafanua jambo wakati watumishi wa Wizara hiyo wakipatiwa mafunzo ya kujikinga na virusi vya Covid19 kutoka kwa wataalam wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto katika ofisi za Wizara hiyo Mtumba Jijini Dodoma. Mtaalam wa Afya kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto akiwaonyesha namna sahihi ya kunawa mikono watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakati akiwapatia mafunzo ya kujikinga na virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Corona.