Posts

Showing posts from June, 2020

MPANJU ATAKA VIPAUMBELE VYA MSINGI VIIBULIWE KATIKA MPANGO KAZI WA PILI WA HAKI ZA BINADAMU

Image
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju akifungua kikao cha siku mbili cha wataalam wa Kikosi kazi cha kupitia rasimu ya mpango kazi wa pili wa haki za binadamu kinachofanyika jijini Dodoma.Wengine pichani kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Haki za Binadamu Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Nkasori Sarakikya na kushoto ni  Afisa Mchunguzi Mkuu na Mratibu wa Mpango kazi wa kwanza wa haki za binadamu Bw. Laurent Buliro kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora. Wataalam wa kikosi kazi cha kupitia rasimu ya mpango kazi wa pili wa haki za binadamu wakimsikiliza mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju (hayupo pichani) wakati akifungua kikao cha kupitia rasimu hiyo. Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju akiwa katika picha ya pamoja na Wataalam wa kikosi kazi cha kupitia rasimu ya mpango kazi wa pili wa haki za binadamu baada ya kufungua kikao chao. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

WIZARA YA KATIBA NA SHERIA YAADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

Image
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Deogratias Yinza akiongea na watumishi wa Wizara hiyo katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoadhimishwa kila mwaka kuanzia tarehe 16 hadi 23, Juni. Katika maadhimisho hayo watumishi hao walikumbushwa kanuni, taratibu na miongozo mbalimbali inayopaswa kufuatwa na watumishi wa Umma. Kauli mbiu ya mwaka huu ni " Jukumu la utumishi wa Umma katika kujenga na kudumisha amani iliyopo miongoni mwa jamii". Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakimsikiliza Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara hiyo Bw. Deogratias Yinza (hayupo pichani) katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma. Afisa Rasilimali Watu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Hilda Makwinya (mwenye kilemba) akiongea na watumishi wa Wizara hiyo katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.

RAIS MAGUFULI AIPONGEZA SEKTA YA SHERIA

Image
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Magufuli aipongeza sekta ya sheria kwa mafanikio iliyoyapata katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Pongezi hizo amezitoa katika hotuba yake ya kufunga Bunge la 11, alisema katika kipindi hicho sekta ya sheria imejitahidi kupunguza vitendo vya rushwa, ucheleweshaji na ubambikaji wa kesi pamoja na mlundikano wa wafungwa . Alisema “ Ili kukabiliana na tatizo la ucheleweshaji wa kesi Serikali iliteua Majaji wapya 17 wa Mahakama ya Rufani, Majaji 52 wa Mahakama Kuu na kuajiri watumishi wa mahakama 859, wakiwemo mahakimu 396”. Aidha, Katika kipindi cha uongozi wa Serikali ya awamu ya tano Mahakama kadhaa zilijengwa na nyingine kukarabatiwa na mahakama inayotembea ilianzishwa katika mikoa ya Dar es salaam na Mwanza, hadi kufikia mwezi wa tatu 2020 ilikuwa imeshasajili mashauri 337 na kusikiliza mashauri 274 hizi zote zikiwa ni jitihada za kupunguza   mlundikano wa

SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

Image