MPANJU ATAKA VIPAUMBELE VYA MSINGI VIIBULIWE KATIKA MPANGO KAZI WA PILI WA HAKI ZA BINADAMU
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju akifungua kikao cha siku mbili cha wataalam wa Kikosi kazi cha kupitia rasimu ya mpango kazi wa pili wa haki za binadamu kinachofanyika jijini Dodoma.Wengine pichani kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Haki za Binadamu Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Nkasori Sarakikya na kushoto ni Afisa Mchunguzi Mkuu na Mratibu wa Mpango kazi wa kwanza wa haki za binadamu Bw. Laurent Buliro kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.
Wataalam wa kikosi kazi cha kupitia rasimu ya mpango kazi wa pili wa haki za binadamu wakimsikiliza mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju (hayupo pichani) wakati akifungua kikao cha kupitia rasimu hiyo.
Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju akiwa katika picha ya pamoja na Wataalam wa kikosi kazi cha kupitia rasimu ya mpango kazi wa pili wa haki za binadamu baada ya kufungua kikao chao.
Wataalam wa kikosi kazi cha kupitia rasimu ya mpango kazi wa pili wa haki za binadamu wakimsikiliza mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju (hayupo pichani) wakati akifungua kikao cha kupitia rasimu hiyo.
Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju akiwa katika picha ya pamoja na Wataalam wa kikosi kazi cha kupitia rasimu ya mpango kazi wa pili wa haki za binadamu baada ya kufungua kikao chao.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju
akitaka kikosi kazi cha wataalam kutoka Wizara na Taasisi za Serikali
zinazopitia rasimu ya Mpango kazi wa pili wa haki za binadamu kuibua vipaumbele
vya msingi ambavyo vimekosekana katika mpango kazi wa kwanza ulioishia 2017.
“Mpango kazi wa kwanza ulioanza 2013 na kuishia 2017
haukuzingatia vipaumbele hivyo mpango kazi huu wa pili ulete vipaumbele vya
msingi”.
Naibu Katibu Mkuu aliyasema hayo wakati akifungua kikao kazi
hicho cha siku mbili kinachofanyika jijini Dodoma.
Aliongeza, kazi hii ya kupitia rasimu ya mpango kazi wa pili
wa haki za binadamu ni muhimu kuifanya kwa umakini kwani inatoa muongozo wa
kisera katika kusimamia masuala ya haki za binadamu na pia hauji kuwa mbadala
wa mambo mengine ya haki za binadamu.
Mpanju aliwasisitiza wataalam hao kuwa mpango kazi huu
uzingatie haki za kiraia, kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni, kijamii, kimaendeleo
na makundi maalum mfano wakulima na walemavu.
Aliongeza, mpango kazi wa pili wa haki za binadamu ni
kipaumbele cha Serikali na utakuwa mwongozo wa kisera wa kukuza na kulinda haki
za binadamu nchini na hivyo alisisitiza kuwa kila taasisi ihakikishe kwamba
vipaumbele katika sekta zao zimo katika mpango kazi huu ili kuufanya uwe bora
zaidi kwani mpango kazi wa haki za binadamu wa kwanza japokuwa ulipata
mafanikio kadhaa lakini haukuzingatia vipaumbele.
Aliwasihi wataalam hao kufanya kazi kwa weledi na kwa kujituma
na kutambua kwamba zoezi hili ni nyeti na ni la muhimu alisema, “nawasihi kutoa
ushirikiano, kufanya kazi kwa weledi, kwa kujituma na kutambua kwamba zoezi
hili ni nyeti na ni la umuhimu kwa kuwa ni mfumo wakuhakikisha Serikali
inatimiza wajibu wake wa kukuza na kulinda haki za binadamu kwa wananchi wake.
Aidha, alizitaka asasi zisizo za Serikali kuweka mfumo mzuri
wa kufuatilia masuala ya haki za binadamu katika Halmashauri hadi Serikali kuu
na kutatua changamoto zilizokuwepo kwenye mpango kazi wa kwanza wa haki za binadamu.
Kabla ya kuandaliwa kwa rasimu hii ya mpango kazi wa pili wa haki za binadamu
maoni mbalimbali yalikusanywa kutoka kwa wadau katika mikoa mbalimbali Tanzania
Bara na Visiwani na hivyo Naibu Katibu Mkuu alikitaka kikosi kazi hicho kuweka
vizuri mawazo hayo kutoka kwa wananchi ili kupata mpango kazi ulio mzuri kwa
Taifa.
Kikosi kazi hiki cha wataalam kimeundwa ili kupitia muongozo
wa kisera unaolenga kutatua changamoto mbalimbali zilizojitokeza kwenye mpango
kazi wa kwanza ambao ulikosa vipaumbele vya msingi.
Comments
Post a Comment