RAIS MAGUFULI AIPONGEZA SEKTA YA SHERIA




XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Magufuli aipongeza sekta ya sheria kwa mafanikio iliyoyapata katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.

Pongezi hizo amezitoa katika hotuba yake ya kufunga Bunge la 11, alisema katika kipindi hicho sekta ya sheria imejitahidi kupunguza vitendo vya rushwa, ucheleweshaji na ubambikaji wa kesi pamoja na mlundikano wa wafungwa . Alisema “ Ili kukabiliana na tatizo la ucheleweshaji wa kesi Serikali iliteua Majaji wapya 17 wa Mahakama ya Rufani, Majaji 52 wa Mahakama Kuu na kuajiri watumishi wa mahakama 859, wakiwemo mahakimu 396”.

Aidha, Katika kipindi cha uongozi wa Serikali ya awamu ya tano Mahakama kadhaa zilijengwa na nyingine kukarabatiwa na mahakama inayotembea ilianzishwa katika mikoa ya Dar es salaam na Mwanza, hadi kufikia mwezi wa tatu 2020 ilikuwa imeshasajili mashauri 337 na kusikiliza mashauri 274 hizi zote zikiwa ni jitihada za kupunguza  mlundikano wa kesi.

Rais Magufuli aliongeza kuwa katika kukabiliana na tatizo la ucheleweshwaji wa kesi alitia saii hati ya kuimarisha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na kuanzishwa kwa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, alisema “uwekaji saini hati hiyo umeongeza tija na kuleta ufanisi mkubwa katika usimamizi na uendeshaji wa mashauri Mahakamani na pia kwenye Mabaraza ya usuluhishi ndani na nje ya nchi.”

Vilevile alisema, Wafungwa 42,774 waliokuwa wakitumikia vifungo mbalimbali walisamehewa na mahabusu 2812 walifutiwa kesi ili kupunguza mlundikano magerezani.

Wakati huohuo, Rais Magufuli alisema mageuzi makubwa yamefanyika kwenye sekta ya madini ambapo Mwezi Julai 2017 sheria ya kulinda Rasilimali za Taifa ikiwemo madini ilipitishwa alisema, “Nashukuru kupitisha sheria hii muhimu sana kwa taifa letu. Kwa hakika mmeingia kwenye vitabu vya historia ya nchi yetu na vizazi vitawakumbuka”

Aliongeza, Kupitishwa kwa sheria hiyo kumewezesha kwa mara ya kwanza Watanzania kumiliki rasilimali zao kwa nguvu za kisheria. Na sheria hiyo pia ndiyo imefanikisha kuanzishwa kwa kampuni ya Twiga Minerals Company ambayo Serikali inamiliki hisa 16% na Barrick 84%. Kadhalika imesaidia kutolewa kwa malipo ya fidia ya dola milioni 100 kati ya dola million 300 ambazo kampuni ya Barrick ilikubali kulipa.

Katika hotuba yake Rais Magufuli alimshukuru Mh. Spika kwa kuunda Kamati maalum ya Bunge ya kuchunguza utoroshaji wa madini ya Tanzanite ambapo Kamati hiyo ilitoa ushauri wa kujenga ukuta wa Km 25 katika mgodi wa Mererani na  Serikali iliujenga kwa haraka sana.

Sekta ya Madini imeanza kukua kwa kasi ambapo 2019 iliongoza kwa ukuaji kwa 17.7% ikifuatiwa na ujenzi 14.1%.

Aliongeza, Mapato yatokanayo na madini nayo yameongezeka, mwaka 2018/2019  zilikusanywa bilioni 346 kutoka bilioni 194 mwaka 2016/17. Mwaka huu 2019/20 bilioni 470 zinatarajiwa kukusanywa ambapo mwezi Aprili 2020 pekee licha ya kuwepo kwa ugonjwa wa corona bilioni 58 zimekusanywa.

Alisema, haijawahi kutokea kabisa, kiwango cha juu kilichowahi kukusanywa kwa mwezi kilikuwa bilioni 43. Haya yametokana na kupitishwa kwa sheria hii.

Rais Magufuli alisema mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitano ni matokeo ya ushirikiano miongoni mwa watanzania wote hivyo hakuna budi kuendelea kushirtikiana kwa lengo la kuiletea nchi maendeleo.

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA