WIZARA YA KATIBA NA SHERIA YAADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Deogratias Yinza akiongea na watumishi wa Wizara hiyo katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoadhimishwa kila mwaka kuanzia tarehe 16 hadi 23, Juni. Katika maadhimisho hayo watumishi hao walikumbushwa kanuni, taratibu na miongozo mbalimbali inayopaswa kufuatwa na watumishi wa Umma. Kauli mbiu ya mwaka huu ni " Jukumu la utumishi wa Umma katika kujenga na kudumisha amani iliyopo miongoni mwa jamii".
Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakimsikiliza Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara hiyo Bw. Deogratias Yinza (hayupo pichani) katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Afisa Rasilimali Watu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Hilda Makwinya (mwenye kilemba) akiongea na watumishi wa Wizara hiyo katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakimsikiliza Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara hiyo Bw. Deogratias Yinza (hayupo pichani) katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Afisa Rasilimali Watu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Hilda Makwinya (mwenye kilemba) akiongea na watumishi wa Wizara hiyo katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Comments
Post a Comment