Posts

Showing posts from July, 2020

WIZARA YA KATIBA YAENDELEA KUIKIJANISHA DODOMA

Image
Mtumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Dina Njovu akisukuma toroli kupeleka miti kwenye mashimo ili iweze kupandwa.   Mtumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Ernest Mbuna akimwagilia maji mti aliopanda katika zoezi la upandaji miti lililofanyika leo katika viwanja vya Wizara hiyo.   Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Deogratias Yinza akichimba shimo kwa ajili ya kupanda ua katika eneo linalozunguka ofisi za Wizara hiyo. Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiwa katika zoezi la upandaji miti na maua katika eneo llinalozunguka ofisi hizo leo Mtumba jijini Dodoma. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Wizara ya Katiba na Sheria yaendelea kuikijanisha Dodoma kwa kupanda miti ya kivuli, matunda na maua katika viwanja   vya Wizara hiyo iliyopo Mtumba Mkoani Dodoma. Zoezi hilo la upandaji miti limekuwa likifanyika mara kwa mara ili kuwezesha viwanja vya wizara hiyo kuwa na mazingira mazuri ya kuvutia. Miti hiyo mbali na kuwapatia kivuli, watu

BURIANI RAIS MSTAAFU BENJAMIN WILLIAM MKAPA

Image

KATIBU MKUU KATIBA NA SHERIA AWATAKA POLISI, MAGEREZA KUHAKIKISHA HAKI ZA MTOTO ZINALINDWA NA KUHIFADHIWA

Image
Katibu Mkuu Wizara ya katiba na Sheria, Prof. Sifuni Mchome (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Mafunzo ya siku nne kwa maafisa wa Jeshi la Polisi na Magereza kutoka katika mikoa ya Iringa na Mbeya kuhusu utoaji wa huduma ya msaada wa kisheria kwa watoto jana katika ukumbi wa Mahakama ya Tanzania Kanda ya Mbeya- jijini Washiriki wa Mafunzo ya siku nne kuhusu utoaji wa huduma ya msaada wa kisheria kwa watoto jana katika ukumbi wa Mahakama ya Tanzania Kanda ya Mbeya- jijini Katibu Mkuu Wizara ya katiba na Sheria, Prof. Sifuni Mchome akitoa hotuba ya ufunguzi wa Mafunzo ya siku nne kwa maafisa wa Jeshi la Polisi na Magereza kutoka katika mikoa ya Iringa na Mbeya kuhusu utoaji wa huduma ya msaada wa kisheria kwa watoto jana katika ukumbi wa Mahakama ya Tanzania Kanda ya Mbeya- jijini Mbeya. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX SERIKALI imewataka Polisi na Magereza nchini kuhakikisha haki na maslahi ya mtoto anayekinzana na sheria zinalindwa

WAZIRI DKT. MWIGULU NCHEMBA AWASILISHA TAARIFA KATIKA KIKAO CHA 66 CHA TUME YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU

Image
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba amewasilisha taarifa juu ya Haki za Binadamu na za Watu Barani Afrika na ugonjwa wa covid- 19 katika Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu. Taarifa hii imewasilishwa kwa njia ya njia ya kikao cha mtandao (video conference) kwa washiriki waliopo Banjul, Gambia Julai 13, 2020. Katika taarifa hiyo Waziri Nchemba amesema ugonjwa wa covid -19 sio tu ni janga la kiafya bali pia ni la kiuchumi na kijamii. Katika kukabiliana na ugonjwa huu nchi ya Tanzania inakabiliana nao kwa kutofunga mipaka ya nchi na kuendelea na shughuli za uzalishaji mali huku wananchi wakipewa elimu na kusisitizwa kufuata njia za kujikinga na maambukizi ya virusi hivyo.   Njia zinazotumika kukabiliana na covid-19 ni pamoja na kutumia dawa za asili katika kuimarisha kinga ya mwili na pia kujifukiza kwa kutumia   majani ya miti mbalimbali maarufu kama nyungu ili kupambana na ugonjwa huo. Vilevile, W

NAIBU KATIBU MKUU AKAGUA HUDUMA ZA ZA UTOAJI MSAADA WA KISHERIA MKOANI TABORA

Image
Viongozi mbalimbali wakimpokea Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba Amon Mpanju (katikati)  kwa ajili ya kuhudhuria hafla fupi ya uzinduzi wa Kamati ya Uratibu wa Huduma ya Msaada wa Kisheria kwa ngazi ya Mkoa wa Tabora jana Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba Amon Mpanju (kushoto) akibadilishana mawazo na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Tabora (Utumishi na Utawala) Hamis Mkunga (kulia)  wakati wa  hafla fupi ya uzinduzi Kamati ya Uratibu wa Huduma ya Msaada wa Kisheria kwa ngazi ya Mkoa wa Tabora jana . Msajili Msaidizi wa Kamati ya Uratibu wa Huduma ya Msaada wa Kisheria kwa ngazi ya Mkoa (LAPS) Mkoa wa Tabora Panin Kerika akiwasilisha taarifa fupi ya hali ya utoaji wa msaada wa kisheria wakati wa  hafla fupi ya uzinduzi Kamati ya Uratibu wa Huduma ya Msaada wa Kisheria kwa ngazi ya Mkoa wa Tabora jana Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba Amon Mpanju (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Uratibu wa Hudum

SERIKALI KUFUTA ADA YA USAJILI KWA WATOA HUDUMA YA MSAADA WA KISHERIA

Serikali inafanyia kazi wazo la kufuta ada ya usajili kwa watoa huduma ya  msaada wa kisheria ili kuhakikisha huduma hiyo inawafikia  wananchi wanyonge na kwa wakati mahali katika maeneo wanayoishi. Kauli hiyo imetolewa jana Mkoani Tabora na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Amon Mpanju wakati akizindua Kamati ya Uratibu wa Huduma ya Msaada wa Kisheria kwa ngazi ya Mkoa. Hatua hiyo inalenga kuhakikisha huduma ya msaada wa kisheria inawafikia wananchi wanyonge kwa wakati ili muda mwingi ambao wangeutumia kuhangaika na kesi wautumie katika shughuli za uzalishaji mali na kukuza uchumi wao na wa taifa kwa ujumla. Pamoja na wazo hilo ni  lazima watoa huduma hao  wakaendelea kuzingatia taratibu nyingine zilizoanishwa katika Sheria na kanuni ili waweze kuwafikia wananchi wanyonge; alisisitiza Mpanju. “Ni vema watoa Huduma ya Msaada wa Kisheria wakasaidia kutatua kwa haraka migogoro ya wananchi wanyonge ili watumie muda mwingi katika uzalishaji badala ya kuwa Ma