WIZARA YA KATIBA YAENDELEA KUIKIJANISHA DODOMA



Mtumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Dina Njovu akisukuma toroli kupeleka miti kwenye mashimo ili iweze kupandwa. 

Mtumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Ernest Mbuna akimwagilia maji mti aliopanda katika zoezi la upandaji miti lililofanyika leo katika viwanja vya Wizara hiyo.  

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Deogratias Yinza akichimba shimo kwa ajili ya kupanda ua katika eneo linalozunguka ofisi za Wizara hiyo.

Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiwa katika zoezi la upandaji miti na maua katika eneo llinalozunguka ofisi hizo leo Mtumba jijini Dodoma.

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Wizara ya Katiba na Sheria yaendelea kuikijanisha Dodoma kwa kupanda miti ya kivuli, matunda na maua katika viwanja  vya Wizara hiyo iliyopo Mtumba Mkoani Dodoma.

Zoezi hilo la upandaji miti limekuwa likifanyika mara kwa mara ili kuwezesha viwanja vya wizara hiyo kuwa na mazingira mazuri ya kuvutia.

Miti hiyo mbali na kuwapatia kivuli, watumishi watapata fursa ya kula matunda mbalimbali wakiwa kazini ikiwemo zabibu ambalo ni zao linalostawi sana mkoani Dodoma.

Aidha Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara hiyo Ndg. Deogratias Yinza amekuwa mstari wa mbele katka kuhamasisha upandaji wa miti  katika maeneo ya viwanja vya Wizara hiyo na hivyo kuwapa mwamko watumishi wa wizara hiyo wa kupanda miti ili kukabiliana na hali ya ukame iliyopo katika Mkoa wa Dodoma.

Zoezi hili la upandaji miti limejumuisha watumishi wote wa Wizara ya Katiba na Sheria.


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA