PROF. MCHOME ATAKA WATANZANIA KUTUMIA VIZURI RASILIMALI ZILIZOPO NCHINI ILI KUJILETEA MAENDELEO


Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome akifungua kikao cha Makatibu Wakuu na Wakuu wa Taasisi cha kujadili Mfumo Jumuishi wa Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Rasilimali za Nchi kilichofanyika jijini Arusha.

Washiriki wakichangia mada katika kikao cha Makatibu Wakuu na Wakuu wa Taasisi cha kujadili Mfumo Jumuishi wa Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Rasilimali za Nchi. 
Washiriki wakiendelea na kikao.


Washiriki wa kikao wakiwa katika picha ya pamoja.

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX


Nchi ya Tanzania imebarikiwa utajiri wa asili na rasilimali asilia ambazo zikitumika ipasavyo nchi na wananchi wake watakuwa na maendeleo ya kiuchumi.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome wakati wa kikao cha Makatibu Wakuu na Wakuu wa Taasisi za Serikali waliokutana jijini Arusha kujadili Mfumo Jumuishi wa Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Rasilimali za nchi.

Profesa Mchome alisema Sheria ya Usimamizi wa Utajiri wa Asili na Maliasilia ilitungwa ili kuweza kusaidia kulinda rasilimali zilizopo nchini ili ziweze kuwanufaisha wananchi wake.

Alisema “Utajiri wa Asili na Maliasilia zinatakiwa zitumike kwa manufaa ya nchi na watu wake na sio kwa manufaa ya nchi za nje, mwaka 2017 tulitunga sheria ambayo ilisaidia kuweka miongozo jinsi gani tuenende katika eneo hilo na jinsi gani watu watafaidi  kutokana na maliasilia zao  na utajiri ambao upo katika nchi yao”.

Alisema, Wawekezaji wadogo wameanza kuongezeka na kufanya shughuli za uzalishaji kwa vibali halali na kwa uhuru bila kukimbizwakimbizwa na hivyo kuongeza pato la nchi.

Profesa Mchome alisisitiza, kwa sasa ardhi inatumika vizuri haitumiki kwa mtu mmoja kushika eneo kubwa bila manufaa yoyote kwa wananchi sasa ardhi inatumika na kuwapatia wananchi manufaa ambayo wanahitaji katika makazi, kilimo na maeneo mengine kwa hiyo malalamiko yameanza kupungua na wananchi wameanza kuwa wamiliki wa ardhi ambao ni utajiri wa asili na mali asilia unaozungumziwa.

Katibu Mkuu wizara ya katiba na sheria ,Profesa Sifuni Mchome amesema kuwa,endapo nchi yetu itazitumia rasilimali tulizonazo itasaidia sana kuharakisha shughuli za maendeleo Kama zilivyo kwa nchi zingine ambazo uchumi wao umeweza kukua kutokana na matumizi mazuri ya rasilimali hizo.

Aidha, Mhadhiri Mwandamizi wa Uchumi Chuo Kikuu cha Dar es Saalam (UDSM),Dokta Abel Kinyondo alisema kuwa,Kuna njia mbili za kuhakikisha wananchi wananufaika na Kodi na tozo mbalimbali zinazotokana na maliasili zetu  serikali inazitumia kwa namna ya kimkakati kuwarudishia wale walioko chini kabisa waweze kunufaika nazo.

Dokta Kinyondo alisema kuwa ,lazima tujue kuwa kwenye kufaidika zaidi na kwenye hela zaidi sio kwenye tozo na Kodi bali wananchi waunganishwe moja kwa moja katika mnyororo wa thamani katika maliasili kwani sehemu kubwa ya mapato inatokana na rasilimali.

Kwa upande wake, Mwakilishi Mkaazi wa UNDP, Bi Christine Musisi ambao ndio wafadhili wa kikao hicho, alisema wapo tayari kushirikiana na Serikali ya Tanzania kuhakikisha rasilimali za nchi zinalindwa na kunufaisha wananchi wake.

 


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA