WIZARA YA KATIBA KUSHIRIKIANA NA UNDP KUJENGA UELEWA KWA WANANCHI JUU YA UTAJIRI WA ASILI NA RASILIMALI ASILIA


 Kikao kati ya Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) cha kujenga uelewa wa jukumu la Wizara kuhusiana na Uangalizi na Usimamizi waUtajiri wa Asili na Rasilimali za nchi chafanyika Wizarani hapo Mtumba, jijini Dodoma.


Wataalam kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) wakifuatilia majadiliano wakati wa kikao chao na Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria.


Mkurugenzi wa kitengo cha Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Rasilimali Asilia cha Wizara ya Katiba na Sheria  Bi Neema Mwanga akielezea jambo wakati wa kikao kati ya  Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).


Bi. Getrude kutoka kitengo cha mazingira UNDP akichangia mada.



Mkurugenzi Idara ya Huduma za Kisheria kwa Umma Bw. Griffin Mwakapeje akichangia mada.


Bw. Godfrey Mulisa kutoka UNDP akichangia mada.


Picha ya pamoja ya Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria na wataalam kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) baada ya kumaliza kikao chao.


XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Serikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria yakubaliana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kujenga uelewa kwa wananchi juu ya kulinda Utajiri wa Asili na Rasilimali Asilia za nchi.

Makubaliano hayo yamefikiwa katika kikao kati ya Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria na Maafisa kutoka UNDP kilichofanyika wizarani hapo Mtumba, jijini Dodoma.

Katika kikao hicho UNDP waliahidi kuandaa andiko ambalo ndilo litakalokuwa muongozo wa namna ya kutoa elimu kwa wananchi waweze kulewa dhana nzima ya utajiri wa asili na rasilimali asilia na namna ambavyo zinaweza kuwaletea maendeleo kwa wao binafsi na nchi pia.

Bw. Godfrey Mulisa ambaye ni mtaalam kutoka UNDP alisema Shirika lao litasaidia kuangalia ni namna gani watashirikiana kuongeza usimamizi wa utajiri wa asili na rasilimali asilia na kuhakikisha faida inapatikana kwa watanzania.

“Kubwa la kuangalia ni kuongeza usimamizi na kuhakikisha faida inapatikana kwa watanzania” alisema Bw. Godfrey

Naye Bi. Getrude kutoka kitengo cha mazingira kwenye shirika hilo alisema UNDP itashirikiana na kitengo cha Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Rasilimali Asilia kilichopo wizarani hapo ili kukijengea uwezo kitengo hicho kiweze kufuatilia rasilimali na utajiri uliopo Tanzania ili kuweza kuinua uchumi wa nchi na wananchi kwani shirika hilo linaangalia sana maendeleo ya watu.

Awali akielezea kuhusu jukumu ililonalo Wizara ya Katiba na Sheria la kusimamia utajiri wa asili na rasilimali asilia Mkurugenzi wa Kitengo cha Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Rasilimali Asilia Bi. Neema Mwanga alisema jukumu kubwa lililonalo ni kuangalia mifumo au mikataba iliyopo inahakikisha inalinda rasilimali za Taifa.

Aliongeza kuwa kitengo hicho kilianzishwa mwaka 2018 ili kuratibu na kuangalia maendeleo endelevu ya uvunaji na matumizi ya utajiri wa asili na rasilimali, pia kusajili na kuangalia mikataba inayohusu rasilimali asilia, na kupitia sheria, sera na miongozo ili zisiathiri matakwa ya Katiba.

Aidha, Mkurugenzi huyo alisisitiza Katiba inahitaji wananchi walinde rasilimali hivyo ni vyema wakapata elimu ya namna ya kulinda kwani uelewa mdogo wa jamii kuhusu sheria ni kikwazo katika kulinda rasilimali asilia.

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA