MKUU WA MKOA WA TANGA ATAKA TAASISI ZA UTOAJI HAKI ZIBORESHWE ILI ZIWEZE KUTOA HAKI KWA WAKATI

 


XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martin Shigella ataka taasisi za utoaji haki ziendelee kuboreshwa ili haki iweze kupatikana kwa wakati.

Mhe. Shigella aliyasema hayo wakati akifungua mafunzo kwa kamati za usalama za mkoa na Wilaya, kamati za maadili ya Mahakimu na Kamati za Parole mkoani Tanga ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria.

Mhe. Mkuu wa Mkoa aliwaambia viongozi hao kuwa wana dhamana kubwa ya kuhakikisha nchi ina utulivu, amani na usalama hivyo waitumie fursa hii ya kupata mafunzo hayo vizuri na kushirikishana na wengine.

“Tuna dhamana kubwa ya kuhakikisha utulivu, usalama na amani ya nchi tunaitimiza kwa Pamoja, tutumie fursa hii vizuri na tushirikishane” alisema Mhe. Shigella.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amesema mamlaka za kutenda haki mkoani humo ikiwemo Mabaraza ya ardhi ya kata yamekuwa yakilalamikiwa sana kutokana na ufanisi wake ambao unasababishwa na watumishi wachache waliopo ambayo inasababisha ucheleweshwaji wa majukumu yao ikiwemo kupatikana kwa nakala za hukumu.

Aliongeza, Mkoani Tanga chama cha wanasheria kimeendelea kutoa msaada mkubwa sana wa kisheria kwa wananchi lakini bado hautoshelezi kwani matatizo ya kisheria ni mengi hivyo awaomba waendelee kujitangaza ili wananchi waweze kuwafahamu na kwenda kupata msaada wa kisheria. Pia aliahidi ofisi za Wakuu wa Wilaya na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa zipo tayari kusaidia gharama ndogondogo ambazo zitahitajika kuendesha kesi za wananchi zinapoenda mahakamani.

“Msaada mnaotoa ni ibada na sehemu ya sadaka kwani unagusa Maisha ya watu wengi tena wengine kutoka mbali na mlipo hivyo mjitahidi kuwasikiliza na kuwasaidia” alisema Mhe.Shigella.

Aidha, Mkuu wa Mkoa alisema mafunzo haya yanayohusisha viongozi wengi wakiwemo mahakimu yamekuja wakati muafaka na wakati serikali ya awamu ya tano muhula wa pili unapoanza hivyo ana imani yatawasaidia katika kutekeleza majukumu yao.

 


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA