WAJUMBE WA MABARAZA YA ARDHI ACHENI KUPOKEA RUSHWA – MHE. NGUVIRA

 


XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

 

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga Mhe. Toba Nguvira awaasa wajumbe wa mabaraza ya ardhi wilayani humo kuacha tabia ya kupokea rushwa na kunyima haki wananchi.

Mhe. Nguvira aliyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya utawala bora, Wosia na Mirathi kwa watendaji kata na wenyeviti wa mabaraza ya ardhi wilayani humu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria ambayo kitaifa yalizinduliwa tarehe 12 Mkoani Tanga.

Mkuu wa wilaya huyo aliwaambia watendaji kata na wenyeviti wa mabaraza ya kata hao wayatumie mafunzo hayo vizuri ili kumaliza migogoro mingi iliyopo ambayo inaanzia kwenye kata na inasababishwa na rushwa na hivyo kunyima haki baadhi ya wananchi.

“Migogoro ya ardhi na mirathi ni mingi sana nchini na inasababishwa na rushwa” alisema Mkuu wa wilaya huyo.

Aidha Mhe. Nguvira alisema sheria zimewekwa kuhakikisha haki inatendeke kwani kukosekana kwa haki kunapelekea machafuko katika jamii.

Mhe. Nguvira aliwasisitiza wajumbe wa mafunzo hayo kuyatendea haki kwa kuyatumia mafunzo watakayopata kuyatafsiri katika mabaraza ya kata.

Aimshukuru Mkuu wa Wilaya kwa nasaha zake kabla ya kuanza kw mafunzo mwezeshaji wa mafunzo hayo amabye pia ni Naibu Katibu kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Bw. Calist Luanda alisema amepewa jukumu la kiutoa mafunzo kwa wajumbe hao hivyo awasisitiza wajumbe kuyafanyia kazi mafunzo watakayopewa ili waweze kuboresha kazi zao na kutoia haki kwa wananchi.


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA