Posts

Showing posts from December, 2020

WANYONGE NI LAZIMA WALINDWE NA SHERIA-DKT MWIGULU

Image
 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akiongea na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Shinyanga alipofanya ziara ya kikazi mkoani humo. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akiongea na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Shinyanga (hawapo pichani)  alipofanya ziara ya kikazi mkoani humo. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. John Pombe Magufuli imejipambanua kuwalinda wanyonge hivyo anapojitokeza mtu yeyote kutaka kuwaumiza ni lazima ashughulikiwe kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.   Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ametoa angalizo hilo tarehe 15 Disemba 2020 wakati akizungumza kwenye kikao kazi na kamati ya ulinzi na usalama ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe Anamringi Macha akiwa katika ziara ya kikazi ya siku moja Mkoani Shinyanga.   Nchemba amekemea vikali wananchi wanaotaka kuijaribu serikali inayoongozwa na Mhe Rais Dkt

ONGEZENI NGUVU KATIKA KUSIMAMIA HAKI ZA WANANCHI - MHE. NCHEMBA

Image
 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Mwigulu Nchemba akiongea na watumishi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (hawapo pichani) alipofanya ziara katika ofisi ya Tume hiyo. Wengine pichani ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo  Mhe. Geoffrey Mizengo Pinda (kulia) na mwingine ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo Ndg. Amon Mpanju. Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe. Mathew Maimu (aliyesimama) akitoa taarifa ya utekelezaji kwa Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Mwigulu Nchemba alipotembelea ofisi za Tume hiyo. Baadhi ya watumishi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora wakimsikiliza Waziri wa Katiba na Sheria alipofanya ziara katika ofisi za Tume hiyo. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Mwigulu Nchemba aitaka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kuongeza nguvu katika kusimamia na kusikiliza malalamiko ya wananchi. Mhe. Nchemba ameyasema hayo alipofanya ziara ya kwanza ya kikazi katika Tume hiyo tangu alipoapishwa kushika wadhifa huo katika