ONGEZENI NGUVU KATIKA KUSIMAMIA HAKI ZA WANANCHI - MHE. NCHEMBA


 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Mwigulu Nchemba akiongea na watumishi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (hawapo pichani) alipofanya ziara katika ofisi ya Tume hiyo. Wengine pichani ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo  Mhe. Geoffrey Mizengo Pinda (kulia) na mwingine ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo Ndg. Amon Mpanju.


Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe. Mathew Maimu (aliyesimama) akitoa taarifa ya utekelezaji kwa Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Mwigulu Nchemba alipotembelea ofisi za Tume hiyo.


Baadhi ya watumishi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora wakimsikiliza Waziri wa Katiba na Sheria alipofanya ziara katika ofisi za Tume hiyo.


XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Mwigulu Nchemba aitaka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kuongeza nguvu katika kusimamia na kusikiliza malalamiko ya wananchi.

Mhe. Nchemba ameyasema hayo alipofanya ziara ya kwanza ya kikazi katika Tume hiyo tangu alipoapishwa kushika wadhifa huo katika awamu ya pili ya serikali ya awamu ya tano.

Mhe. Nchemba alisema “changamoto kwa wananchi zinaendelea kukua hivyo ongezeni nguvu katika kazi yenu ya kusikiliza malalamiko yao”

Aliongeza, Tume inatakiwa iwafikie wananchi kule waliko   na waangalie maeneo ambayo wananchi wanakosa haki zao ili waweze kuwatembelea na kutatua changamoto zinazowakabili na kuwawzesha kupata haki hizo kwani maeneo mengi kuna uonevu mwingi na wanyonge kuporwa haki zao.

Alisisitiza kuwa eneo la haki za watu likifanyiwa kazi ipasavyo litasaidia wananchi kuzipata haki hizo kwani Tanzania ni taifa huru hivyo Tume inapaswa kujali wananchi na kuwahudumia wote kwa usawa.

Waziri aliongeza kuwa masuala ya haki za binadamu ni kipaumbele cha Serikali ya awamu ya tano hivyo wasitumie vichaka vya haki kutikisa haki za wananchi ni lazima maslahi ya nchi na wananchi yatangulizwe mbele.

Aidha, nae Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Geoffrey Mizengo Pinda alisema Tume ni taasisi iliyoundwa kusaidia jamii lakini kuna watu wanaotaka kupotosha uwepo wake hivyo Tume ya Haki za Binadamu iende kwa jamii ili waweze kuitambua na iwe rahisi kwao kuweza kuisaidia jamii hiyo.

Awali wakati akitoa taarifa ya utekelezaji kwa Mawaziri hao Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe. Mathew Maimu alisema Tume imekuwa ikifanya kazi mbalimbali za kusaidia upatikanaji wa haki kwa jamii japokuwa imekuwa ikikabiliwa na uhaba mkubwa wa majengo ya ofisi na vitendea kazi.


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA