Posts

Showing posts from January, 2021

WATUMISHI WIZARA YA KATIBA WAJENGEWA UWEZO KUHUSU UANGALIZI WA UTAJIRI WA ASILI NA MALIASILIA

Image
 Mkurugenzi Idara ya Huduma za Kisheria Bw. Griffin Mwakapeje akifungua mafunzo ya siku mbili ya kujengea uwezo watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria katika eneo la Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Maliasilia za nchi katika ukumbi wa VETA jijini Dodoma. Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo. Mtoa mada kutoka shirika la Petroli la Taifa (TPDC) Dkt. Elias akitoa mada kwa washiriki wa mafunzo. Picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa mafunzo. XXXXXXXXXXXXXXX Kitengo cha Uangalizi wa Utajiri  wa Asili na Maliasilia kimeandaa mafunzo ya siku mbili kwa watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria ili kuwajengea uwezo kuhusu masuala ya Uangalizi wa Utajiri na Maliasilia. Mafunzo hayo yaliyofunguliwa na mwakilishi wa Katibu Mkuu ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Kisheria Bw. Griffin Mwakapeje ambapo alisema mwaka 2017 Serikali iliwasilisha Bungeni miswada ya kutunga sheria mbili za usimamizi wa maliasilia za nchi. Alisema, hatua za kutunga sheria hizi mbili zilipelekea kujenga uelewa wa pa

WAZIRI MWIGULU APONGEZA UONGOZI WA MAHAKAMA KWA KUTOA USHIRIKIANO NA KUWAPA NGUVU TAWJA KUFANIKISHA KAZI ZAO

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba akisisitiza jambo  wakati akimuwakilisha   Mhe Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania    akifungua  Mkutano Mkuu wa  Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake ( TAWJA )  uliofanyika tarehe 7 Januari 2021 katika ukumbi wa Benki Kuu (BOT) Jijini Mwanza. Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Geofrey Pinda akisisitiza jambo  wakati wa  Mkutano Mkuu wa  Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake ( TAWJA )  uliofanyika tarehe 7 Januari 2021 katika ukumbi wa Benki Kuu (BOT) Jijini Mwanza. Mgeni rasmi-Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa   Mkutano Mkuu wa  Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake ( TAWJA )  uliofanyika tarehe 7 Januari 2021 katika ukumbi wa Benki Kuu (BOT) Jijini Mwanza. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba akikabidhiwa Tuzo na Mwenyekiti wa Chama cha Majaji na Mahakimu wanawake (TAWJA) Mhe Jaji Joaquuine De-Mello kwa kut

WAKILI WA SERIKALI MWANDAMIZI WIZARA YA KATIBA NA SHERIA ATUNUKIWA SHAHADA YA UZAMIVU

Image
  Wakili wa Serikali Mwandamizi kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Anne George Malipula ametunukiwa shahada ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA DKT. MWIGULU AAGIZA RITA KUHAMIA DODOMA

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba akisisitiza jambo wakati akizungumza na watumishi wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) akiwa katika ziara ya kikazi. Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Geofrey Mizengo Pinda akisisitiza jambo wakati akizungumza na watumishi wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) wakati alipoandamana na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt Mwigulu Nchemba katika ziara ya kikazi. Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa  Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA)  Bi Emmy Hudson akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Wakala mbele ya Waziri na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria mara baada ya kuwasili kwenye ofisi za wakala kwa ajili ya ziara ya kikazi. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba pamoja na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Geofrey Mizengo Pinda wakikagua maktaba ya kumbukumbu za vyeti vya kuzaliwa na vifo wakati walipotembelea ofisi za Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) wakiwa katika ziara ya kikazi. S

SHERIA, MWENENDO WA MASHAURI NA HUKUMU ZIANDIKWE KWA LUGHA YA KISWAHILI – DKT MWIGULU NCHEMBA

Image
Waziri wa katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba akisisitiza jambo wakati akizungumza na Menejimenti ya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (Law School of Tanzania) alipofanya ziara katika taasisi hiyo .   Waziri wa katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba akisisitiza jambo wakati akizungumza na Menejimenti ya Taasisi ya mafunzo ya uanasheria kwa vitendo Tanzania (Law School of Tanzania) . Waziri wa katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba akikagua maktaba ya Taasisi ya mafunzo ya uanasheria kwa vitendo Tanzania (Law School of Tanzania) . Naibu Waziri wa katiba na Sheria Mhe Geofrey Mizengo Pinda akisisitiza jambo wakati akizungumza na Menejimenti ya Taasisi ya mafunzo ya uanasheria kwa vitendo Tanzania (Law School of Tanzania) alipofanya ziara ya kikazi hivi karibuni. Mkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (Law School of Tanzania) Jaji Dkt. Benhajj Masoud akimkaribisha waziri wa Katiba na  Sheria Dkt. Mwigulu Nchemba (hayupo pichani) kuzun

WAZIRI MWIGULU NCHEMBA AIPONGEZA MAHAKAMA KWA UFANISI

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye kikao kazi na Menejimenti ya Mahakama akiwa katika ziara ya kikazi jijini Dar Es Salaam . Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba (Wa Pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na  Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Jaji Prof. Ibrahim Khamis Juma (Wa Pili Kushoto), Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Geofrey Mizengo Pinda (Kushoto) na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi (Kulia)  mara baada ya kufanya mazungumzo na Menejimenti ya Mahakama. Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Ernest Mchome akifuatilia hotuba ya Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba (hayupo pichani) akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye kikao kazi na Menejimenti ya Mahakama.  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba akifuatilia taarifa ya utekelezaji wa maboresho ya mahakama pamoja na taarifa ya usikilizaji wa mashauri wakati wa kikao ka