SHERIA, MWENENDO WA MASHAURI NA HUKUMU ZIANDIKWE KWA LUGHA YA KISWAHILI – DKT MWIGULU NCHEMBA

Waziri wa katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba akisisitiza jambo wakati akizungumza na Menejimenti ya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (Law School of Tanzania) alipofanya ziara katika taasisi hiyo.

 

Waziri wa katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba akisisitiza jambo wakati akizungumza na Menejimenti ya Taasisi ya mafunzo ya uanasheria kwa vitendo Tanzania (Law School of Tanzania).


Waziri wa katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba akikagua maktaba ya Taasisi ya mafunzo ya uanasheria kwa vitendo Tanzania (Law School of Tanzania).


Naibu Waziri wa katiba na Sheria Mhe Geofrey Mizengo Pinda akisisitiza jambo wakati akizungumza na Menejimenti ya Taasisi ya mafunzo ya uanasheria kwa vitendo Tanzania (Law School of Tanzania) alipofanya ziara ya kikazi hivi karibuni.


Mkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (Law School of Tanzania) Jaji Dkt. Benhajj Masoud akimkaribisha waziri wa Katiba na  Sheria Dkt. Mwigulu Nchemba (hayupo pichani) kuzungumza na watumishi wa taasisi hiyo alipofanya ziara ya kikazi hivi karibuni.


XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Serikali imedhamiria kuwasaidia kwa umakini mkubwa wananchi katika tasnia ya sheria ambapo imeagiza kuanza haraka uandaaji wa sheria kwa lugha ya kiswahili ikiwemo mwenendo wa mashauri na hukumu.

 

Agizo hilo kwa katibu mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria limeelekeza kutafutwa haraka iwezekanavyo wataalamu watakaozitafsiri sheria zote zilizoandikwa kwa lugha ya kingereza na kuwa katika lugha ya Taifa ya kiswahili.

 

Waziri wa katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba ametoa agizo hilo tarehe 22 Disemba 2020 alipotembelea Taasisi ya mafunzo ya uanasheria kwa vitendo Tanzania (Law School of Tanzania) wakati akiwa katika siku ya pili ya ziara ya kikazi Jijini Dar es salaam.

 

"Kwenye kauli nzuri za kuvutia tunasema kiswahili ndio lugha nzuri tena ya kuvutia hivyo ni lazima tuanze kufundisha kwa kufuata muelekeo wa lugha ya Taifa ili kuachana na utumwa wa matumizi ya lugha za kikoloni katika sheria zetu" Amekaririwa Mhe Nchemba

 

Amesema kuwa Sheria ambayo mwananchi anahukumiwa imeandikwa kingereza, hukumu anayopewa imeandikwa katika lugha ya kingereza hilo ni eneo la haki za watu hivyo inapaswa kwanza lugha ya kiswahili ndiyo itumike kwenye sheria kisha lugha zingine kama kingereza ziwe nyongeza.

 

Dkt Mwigulu amesema kuwa Sheria zinaandikwa katika lugha ya kingereza na kuwaambia wananchi kutokujua kwao sheria sio sehemu ya utetezi jambo hilo ni kinyume na utaratibu hivyo lazima kufanya mapitio ya sheria zilizopo.

 

"Zipo nchi nyingi Duniani zimeendelea pasina kuwa zinajua lugha ya kingereza hivyo ni wajibu wetu sasa rasmi kuitumia lugha ya kiswahili" Amesisitiza

 

Waziri Mwigulu amesema kuwa katika mikutano mingi ya usaili wa kazi inatumika lugha ya kingereza wakati huo huo viongozi wakuu wa usaili wanatumia lugha ya kiswahili katika familia zao, na hata kazini.

 

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Geofrey Mizengo Pinda amesema kuwa uhitaji wa wataalamu wa kisheria katika maeneo mengi ni mkubwa hivyo taaluma hiyo inapaswa kutolewa kwa weledi mkubwa kwa maslahi makubwa ya Taifa.

 

Amesema kuwa mahitaji ya msaada wa kisheria ni makubwa hivyo ni muhimu kuona ulazima wa kutembelea katika maeneo mbalimbali hususani vijijini kutoa msaada wa kisheria kwani kumekuwa na manyanyaso kwa wananchi wengi.

 

Ameongeza kuwa Taasisi ya mafunzo ya uanasheria kwa vitendo Tanzania ni sehemu ya ukombozi kwa wananchi hivyo kuna kila sababu ya kutengeneza chombo kama hicho kuwafikia wananchi kirahisi.

 


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA