WATUMISHI WIZARA YA KATIBA WAJENGEWA UWEZO KUHUSU UANGALIZI WA UTAJIRI WA ASILI NA MALIASILIA
Mkurugenzi Idara ya Huduma za Kisheria Bw. Griffin Mwakapeje akifungua mafunzo ya siku mbili ya kujengea uwezo watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria katika eneo la Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Maliasilia za nchi katika ukumbi wa VETA jijini Dodoma.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo.
Mtoa mada kutoka shirika la Petroli la Taifa (TPDC) Dkt. Elias akitoa mada kwa washiriki wa mafunzo.
Picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa mafunzo.Kitengo cha Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Maliasilia kimeandaa mafunzo ya
siku mbili kwa watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria ili kuwajengea uwezo kuhusu
masuala ya Uangalizi wa Utajiri na Maliasilia.
Mafunzo hayo yaliyofunguliwa na mwakilishi wa Katibu Mkuu
ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Kisheria Bw. Griffin Mwakapeje
ambapo alisema mwaka 2017 Serikali iliwasilisha Bungeni miswada ya kutunga
sheria mbili za usimamizi wa maliasilia za nchi.
Alisema, hatua za kutunga sheria hizi mbili zilipelekea
kujenga uelewa wa pamoja juu ya maliasilia pasipo kuingilia majukumu ya wizara
au taasisi nyingine.
Aliongeza kuwa baada ya kutunga sheria wizara iliunda
kitengo kwa ajili ya kuratibu ili kuhakikisha watu wote wanajumuika kulinda maliasilia
ambapo matokeo baada ya kutungwa kwa sheria hizo ni kujengwa kwa ukuta wa
Mererani ili kudhibiti utoroshwaji wa madini, kuanzishwa soko la madini ili
wananchi wanufaike na masoko, kuibuka kwa watanzania ambao ni mabilionea na
kuanzishwa viwanda vya uchenjuaji.
Mafunzo hayo yalitolewa na Shirika la Petroli la Taifa
(TPDC), Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Maliasili na Utalii na Wizara ya
madini.
Comments
Post a Comment