WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA DKT. MWIGULU AAGIZA RITA KUHAMIA DODOMA
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba akisisitiza jambo wakati akizungumza na watumishi
wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) akiwa katika ziara ya
kikazi.
Naibu Waziri wa Katiba na
Sheria Mhe Geofrey Mizengo Pinda akisisitiza jambo wakati akizungumza na watumishi
wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) wakati alipoandamana
na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt Mwigulu Nchemba katika ziara ya kikazi.
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu
wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) Bi Emmy Hudson akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Wakala mbele ya Waziri na Naibu
Waziri wa Katiba na Sheria mara baada ya kuwasili kwenye ofisi za wakala kwa ajili ya ziara ya kikazi.
Waziri wa Katiba na Sheria
Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba pamoja na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Geofrey
Mizengo Pinda wakikagua maktaba ya kumbukumbu za vyeti vya kuzaliwa na vifo
wakati walipotembelea ofisi za Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA)
wakiwa katika ziara ya kikazi.
Sehemu ya watumishi
wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA), Wizara ya Katiba na
Sheria pamoja na Waandishi wa Habari wakifuatilia hotuba ya Waziri wa
Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba akisisitiza jambo wakati akiwa
katika ziara ya kikazi kwenye ofisi za Wakala jijini Dar Es Salaam.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Serikali
imeitaka Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) wenye maskani
yake Jijini Dar es salaam kuanza mchakato wa haraka kuhakikisha unahamia Jijini
Dodoma.
Agizo
hilo limetolewa na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba tarehe
21 Disemba 2020 wakati akizungumza na watumishi wa taasisi hiyo akiwa katika
ziara ya kikazi Jijini Dar es salaam.
Waziri
Mwigulu amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. John
Pombe Magufuli ametoa maelekezo ya serikali kuhamia Jijini Dodoma hivyo taasisi
zote zinapaswa kuhamia haraka iwezekanavyo.
“Bahati
nzuri mmeniambia kuwa mna kiwanja Jijini Dodoma hivyo safari ya Dodoma
inawahusu ni lazima mhamie Dodoma, zile Taasisi zinazochelewa kuhamia Dodoma
itafikia wakati tutafanya uamuzi wa kuziuza mkiwa ndani ya ofisi” Amekaririwa
Dkt Mwigulu
Waziri
Mwigulu amemuagiza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa RITA pamoja na Afisa
Mtendaji Mkuu wa RITA kuhakikisha kuwa wanaweka mkazo kuhakikisha taasisi hiyo
inahamia Dodoma haraka iwezekanavyo.
Ameongeza
kuwa Rais Magufuli ameonyesha mfano kwa kujenga Ikulu ya Chamwino inayofanana
na Ikulu ya Jijini Dar es salaam huku tayari akiwa amehamia Jijini Dodoma hivyo
taasisi hiyo ni muhimu kuhamia Dodoma.
“Binafsi
sitopenda ikifanyika sensa ya Taasisi ambazo zinastahili kuhamia Dodoma halafu
zikutwe bado zipo Jijini Dar es salaam zikiwemo taasisi za Wizara ya Katiba na
Sheria”
Kadhalika
ameagiza kuhakikisha kuwa watendaji wa taasisi ya RITA wanatembelea mara kwa
mara Jijini Dodoma katika shughuli za kikazi ili kuendelea kuzoea Jiji hilo
wakati wanafanya maandalizi ya kuhama.
Kwa
upande wake Naibu Waziri wa Katiba na sheria Mhe Geofrey Mizengo Pinda ameitaka
taasisi hiyo kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi ili kurahisisha utendaji kazi
kadhalika kuongeza uwezekano wa kujitangaza katika vyombo mbalimbali vya habari.
Pinda
ameongeza kuwa serikali imekusudia kuimarisha upatikanaji wa huduma kwa
wananchi hivyo RITA inapaswa kuongeza urahisi wa upatikanaji wa huduma hususani
katika utoaji wa vitambulisho kwa ngazi ya majimbo.
Awali
akitoa taarifa ya Taasisi hiyo, Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa
Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) Bi Emmy Hudson amesema kuwa taasisi
hiyo ipo katika mpango mkakati wa kuharakisha ufungaji wa mirasi kwa wakati
pamoja na kuboresha mazingira ya uwekezaji na ufanyaji biashara kwa kuhakikisha
sheria ya ufilisi inakamilika na kupitishwa na bunge.
Sambamba
na hayo amezitaja changamoto mbalimbali zinazoikumba taasisi hiyo ikiwemo
kushindwa kuongeza ada ya utoaji wa vyeti vya kuzaliwa pamoja na upungufu wa
watumishi kwani waliopo ni 203 kati ya 361 wanaohitajika.
Comments
Post a Comment