Posts

Showing posts from February, 2021

KIKAO CHA KUCHAMBUA TAKWIMU ZA MCHANGO WA UTAJIRI WA ASILI NA MALIASILIA ZA NCHI KATIKA PATO LA TAIFA

Image
Wajumbe wa kikao kazi cha wataalam wa ndani na nje ya wizara wakijadili jinsi ya kuchambua takwimu za mchango wa Utajiri wa Asili na Maliasilia za Nchi katika pato la Taifa. Wataalam hao wanatoka Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Fedha na Mipango, Wakala wa Serikali Mtandao, Ofisi ya Taifa ya Takwimu, ESRF, REPOA na Baaza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi. Sehemu ya wajumbe wa kikao kazi cha wataalam wa ndani na nje ya wizara wakijadili jinsi ya kuchambua takwimu za mchango wa Utajiri wa Asili na Maliasilia za Nchi katika pato la Taifa. Mkurugenzi wa Kitengo cha Uangalizi wa Utajiri Asilia na Maliasilia za nchi Bi. Neema Mwanga akisisitiza jambo katika kikao kazi cha wataalam wa ndani na nje ya wizara wakijadili jinsi ya kuchambua takwimu za mchango wa Utajiri wa Asili na Maliasilia za Nchi katika pato la Taifa. Mjumbe wa kikao kazi cha wataalam kujadili jinsi ya kuchambua takwimu za mchango wa Utajiri wa Asili na Maliasilia za Nchi katika pato la Taifa Bw. Emanoel Alfred am

WANANCHI WAASWA KUANDIKA WOSIA KUEPUKA MIGOGORO NDANI YA FAMILIA

Image
  Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Geophrey Pinda akizungumza kwenye semina ya kujenga uelewa kwa Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kwenye masuala ya Utajiri Asilia na Maliasilia za Nchi na Wosia na Mirathi. Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju akizungumza katika  semina ya kujenga uelewa kwa Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kwenye masuala ya Utajiri Asilia na Maliasilia za Nchi na Wosia na Mirathi. Mwenyekiti wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Mhe. Mohamed Mchengerwa akizungumza  kwenye semina ya kamati hiyo kwenye masuala ya Utajiri Asilia na Maliasilia za Nchi na Wosia na Mirathi. Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA Bi. Emmy Hudson akizungumza katika  semina ya kujenga uelewa kwa Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kwenye masuala ya Utajiri Asilia na Maliasilia za Nchi na Wosia na Mirathi. Wajumbe wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria wakifuatilia mada zilizo

SERIKALI HAINA SHERIA KANDAMIZI, SHERIA ZOTE ZINAZOTUMIKA NCHINI ZIMETUNGWA NA BUNGE – MHE. GEOFREY PINDA

Image
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Geophrey Pinda akijibu maswali bungeni wakati wa mkutano wa 12 Jijini Dodoma, Leo tarehe 5 Februari 2021. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX  Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Geophrey Pinda amewahakikishia watanzania kuwa Serikali haina Sheria Kandamizi hivyo Sheria zote zinazotumika nchini zilitungwa na Bunge tukufu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambalo halijawahi kutunga Sheria Kandamizi. Amesema kuwa Serikali kwa kuzingatia mahitaji ya wakati na watu wake, imekuwa ikiwasilisha mapendekezo ya marekebisho ya Sheria mbalimbali ili kuziboresha Sheria hizo. Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe Zainab Katimba aliyetaka kufahamu Serikali ina mpango gani wa kurekebisha baadhi ya sheria kandamizi kwa wanawake ili ziendane na wakati, Mhe Pinda amesema kuwa Kutokana na wakati uliopo na mahitaji ya sasa Serikali imeanzisha mchakato wa kuzipitia baadhi ya sheria ili ziweze kufanyiwa marekebisho kuendana na wakati. Amesema Serikali kupitia Wizara

RAIS MAGUFULI ASISITIZA KUHARAKISHWA KWA MATUMIZI YA KISWAHILI MAHAKAMANI

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Magufuli akizungumza wakati wa sherehe ya maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini iliyofanyika kitaifa jijini Dodoma Februari 01,2021. Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Juma akitoa hotuba yake kwa viongozi na wananchi waliohudhuria sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Sheria na miaka 100 ya Mahakama Kuu ya Tanzania. Baadhi ya viongozi na wananchi waliohudhuria sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Sheria na Miaka 100 ya Mahakama Kuu ya Tanzania. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametoa rai kwa Mhimili wa Mahakama kuweka mkakati wa kutumia lugha ya Kiswahili Mahakamani kwa manufaa ya wananchi huku akimpongeza na kumteua Jaji Zephrine Galeba kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kwa kuonyesha uzalendo wa kuandika hukumu kwa kutumia Kiswahili. Rais Magufuli ambaye alikuwa mgeni rasmi katika sherehe za maadhimisho ya siku ya sheria nchini yaliyofanyika kitaifa jijini Dodoma, alisema

VIONGOZI MBALIMBALI WALIOTEMBELEA BANDA LA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA KATIKA MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA

Image
 Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Prof. Adelardus Kilangi akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Wizara ya Katiba na Sheria katika maadhimisho ya Wiki ya Sheria na Miaka 100 ya Mahakama Kuu. Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Geophrey Mizengo Pinda akimuelekeza jambo Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Kisheria kwa Umma Bw. Griffin Mwakapeje alipotembelea banda la Wizara ya Katiba na Sheria katika maadhimisho ya Wiki ya Sheria na Miaka 100 ya Mahakama Kuu. Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Geophrey Mizengo Pinda akisaini kitabu cha wageni  alipotembelea banda la Mahakama Kuu katika maadhimisho ya Wiki ya Sheria na Miaka 100 ya Mahakama Kuu.  Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani Mhe. Jaji Stephen Magoiga akipata maelezo kutoka kwa watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria alipotembelea banda la Wizara ya Katiba na Sheria  katika maadhimisho ya Wiki ya Sheria na Miaka 100 ya Mahakama Kuu.  Kaimu Mtendaji Mkuu RITA akisaini kitabu cha wageni  alipotembelea banda la Wizara ya Kati

TUMIENI MITANDAO YA SIMU KUELIMISHA MASUALA YA KISHERIA - MAKAMU WA RAIS

Image
 Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki matembezi ya maadhimisho ya Wiki ya Sheria na miaka 100 ya Mahakama Kuu. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Dkt. Mwigulu Nchemba, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Ibrahim Juma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome wakifurahia jambo wakati wa matembezi ya maadhimisho ya Wiki ya Sheria na miaka 100 ya Mahakama Kuu. Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakishiriki matembezi ya maadhimisho ya Wiki ya Sheria na miaka 100 ya Mahakama Kuu. Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakifuatilia hotuba ya Makamu wa Rais wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria na Miaka 100 ya Mahakama Kuu.  Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome (waliokaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa wizara hiyo baada ya uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria na Miaka 100 ya Mahakama Kuu. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassa