WANANCHI WAASWA KUANDIKA WOSIA KUEPUKA MIGOGORO NDANI YA FAMILIA

 

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Geophrey Pinda akizungumza kwenye semina ya kujenga uelewa kwa Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kwenye masuala ya Utajiri Asilia na Maliasilia za Nchi na Wosia na Mirathi.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Ndg. Amon Mpanju akizungumza katika  semina ya kujenga uelewa kwa Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kwenye masuala ya Utajiri Asilia na Maliasilia za Nchi na Wosia na Mirathi.


Mwenyekiti wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Mhe. Mohamed Mchengerwa akizungumza  kwenye semina ya kamati hiyo kwenye masuala ya Utajiri Asilia na Maliasilia za Nchi na Wosia na Mirathi.


Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA Bi. Emmy Hudson akizungumza katika  semina ya kujenga uelewa kwa Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kwenye masuala ya Utajiri Asilia na Maliasilia za Nchi na Wosia na Mirathi.


Wajumbe wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa kwao katika semina ya kuwajengea uelewa juu ya masuala ya Utajiri Asilia na Maliasilia za Nchi na Wosia na Mirathi.

Picha ya pamoja baada ya semina.

XXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria imetoa wito kwa wananchi kuandika  na kuhifadhi wosia katika taasisi ya RITA ili kuepuka migogoro ndani ya familia.

Kamati hiyo inayoongozwa na Mhe. Mohamed Mchengerwa imeona kuwa migogoro mingi inayosababishwa na ndugu kulazimisha kurithi mali za marehemu kinyume na taratibu na sheria zinazosimamia masuala ya mirathi inasababishwa na kutokuwepo na wosia.

Akizungumza katika kikao cha kamati hiyo jijini Dodoma Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Mohamed Mchengerwa amewahimiza wabunge wote ambao bado hawajaandika wosia kufanya hivyo ikiwa kama sehemu ya kuwahamasisha wananchi wao kuchukua hatua mapema na kulifanya jambo hilo kuwa ni kipaumbele kwani migogoro na kesi nyingi zinazohusu mirathi zinatokea katika majimbo yao na kwa kiasi kikubwa huchangiwa  na kutoachwa muongozo unaoelezea mgawanyo wa mali za marehemu.

Alisema "kwa kiasi kibubwa migogoro mingi hutokea na ukifuatilia chanzo chake unabaini kinasababishwa na kutoachwa muongozo unaotoa maelekezo kuhusu mgawanyo wa mali za marehemu" alisema Mhe. Mchengerwa.

Aidha katika kikao hicho Kamati hiyo pia ilipata nafasi ya kujengewa uelewa juu ya kitengo kipya kilichoanzishwa wizarani cheny jukumu la kusimamia Utajiri Asilia na Maliasilia za nchi

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA