Posts

Showing posts from April, 2021

MHE. PROF. KABUDI AKUTANA NA MWAKILISHI MKAAZI WA UN WOMEN

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi akipokea zawadi kutoka kwa Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Wanawake (UN Women) Hodan Addouh alipomtembelea ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma.    Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi akifanya mazungumzo na Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Wanawake (UN Women) Hodan Addouh (wa pili kushoto) alipomtembelea ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma.  Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Wanawake (UN Women) Hodan Addouh (wa pili kulia) alipomtembelea ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma. Miongoni mwa mambo waliyojadiliana Waziri Kabudi na mgeni wake ni pamoja na shirika hilo kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Katiba na Sheria katika masuala ya utoaji msaada wa kisheria, mimba za utotoni na ndoa katika umri mdogo. Na Wazir

KAMISHENI YA AFRIKA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAIPONGEZA TANZANIA KWA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Prof.Palamagamba Kabudi,akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma mara baada ya kumaliza kuwasilisha ripoti ya haki za binadamu katika kikao cha 68 cha Kamisheni ya Afrika ya Haki za binadamu na Watu uliofanyika kwa njia ya Mtandao. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Tanzania imewasilisha ripoti ya haki za binadamu kwenye kikao cha 68 cha Kamisheni ya Afrika ya haki za binadamu na watu, huku kamisheni hiyo ikiipongeza kwa kupiga hatua kubwa katika kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wananchi hasa suala la kusambaza umeme vijijini. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho kilichofanyika kwa njia ya mtandao kikijumuisha nchi zote wanachama na makao Makuu ya kamisheni ambayo ni nchi ya Gambia, Waziri wa Katiba na sheria Prof. Palamagamba Kabudi, amesema kuwa mara baada ya mawasilisho hayo Kamisheni imeipongeza Tanzania kwa kupiga hatua kubwa katika miradi ya maendeleo ambayo inagusa wananchi m

Mhe. GEOPHREY PINDA AONGOZA KIKAO CHA WAKUU WA TAASISI KUPITIA HOTUBA YA BAJETI YA 2021/2022

Image
 Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Geophrey Pinda (kushoto) akiongoza kikao cha Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara kupitia hotuba ya bajeti ya wizara ya mwaka wa fedha 2021/2022. Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Geophrey Pinda akiongoza kikao cha Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara kupitia hotuba ya bajeti ya wizara ya mwaka wa fedha 2021/2022.

WAZIRI KABUDI AWATAKA WATUMISHI KUWA WAZALENDO WA NCHI YAO

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi akifungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Katiba na Sheria. Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi akiongea katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo.  Naibu Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria Mhe. Geophrey Pinda akifafanua jambo katika mkutano wa  Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo.  Picha ya pamoja ya Waziri Kabudi na wajumbe wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi. Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi.  

WAZIRI NCHEMBA AKABIDHI OFISI KWA WAZIRI KABUDI

Image
 Aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba akimkabidhi nyaraka mbalimbali Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi ikiwa ni ishara ya kumkabidhi rasmi ofisi baada ya Mhe. Kabudi kuteuliwa kuiongoza wizara hii.

WAZIRI KABUDI APOKELEWA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi alipowasili wizarani hapo na kupokelewa na viongozi na watumishi wa wizara hiyo mara baada ya kuapishwa kushika wadhifa huo baada ya mabadilikio madogo ya Baraza la Mawaziri yaliyofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan. Waziri Kabudi akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Sifuni Mchome. Waziri Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria.   Waziri Kabudi (wa pili kulia) akisaini kitabu cha wageni alipoingia ofisini kwake.