MHE. PROF. KABUDI AKUTANA NA MWAKILISHI MKAAZI WA UN WOMEN

Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi akipokea zawadi kutoka kwa Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Wanawake (UN Women) Hodan Addouh alipomtembelea ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma. 
 
Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi akifanya mazungumzo na Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Wanawake (UN Women) Hodan Addouh (wa pili kushoto) alipomtembelea ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma. 

Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Wanawake (UN Women) Hodan Addouh (wa pili kulia) alipomtembelea ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma.

Miongoni mwa mambo waliyojadiliana Waziri Kabudi na mgeni wake ni pamoja na shirika hilo kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Katiba na Sheria katika masuala ya utoaji msaada wa kisheria, mimba za utotoni na ndoa katika umri mdogo.

Na Waziri Kabudi ameahidi kumpa ushirikiano wa kutosha na kushirikiana na Wizara na Taasisi nyingine katika yale yote yatakayohitajika ambayo Shirika hilo linayaunga mkono.


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA