KILA MTANZANIA ANA HAKI YA KUPATA TAARIFA – WAZIRI KABUDI
Waziri
wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, akizungumza na wawakilishi
wa Umoja wa Haki ya Kupata Taarifa katika kikao kilichofanyika ofisini kwake Mtumba, jijini
Dodoma.
Mwenyekiti
wa Umoja wa Haki ya Kupata Taarifa Bw. Kajubi Mukajanga akizungumza kwenye
kikao chao na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi katika kikao
kilichofanyika jijini Dodoma.
Baadhi
ya washiriki wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof.
Palamagamba Kabudi, (hayupo pichani) wakati akizungumza na wawakilishi wa Umoja
wa Haki ya Kupata Taarifa katika kikao kilichofanyika jijini Dodoma.
XXXXXXXXXXXXXXXXXX
Waziri
wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi,amewataka watanzania na vyama
visivyo vya kiserikali kulinda haki za binadamu na kufuata sheria za uhuru wa
kujieleza kwani ni jukumu lao kikatiba.
Pia amesema kuwa jukumu la serikali ni
kuhakikisha inasimamia na kuzilinda sheria hizo kupitia taasisi ya tume ya haki
za binadamu na utawala bora.
Waziri.Kabudi ameyasema hayo jijini Dodoma
wakati akizungumza na wawakilishi wa Umoja wa Haki ya Kupata Taarifa.
Amesema katika kuhakikisha kila Mwananchi
anakuwa na uhuru wa kupata habari serikali imeridhia mkataba wa Afrika wa mwaka1981
ambapo ibara ya 9 inaeleza kwamba kila mtu ana haki ya kupata taarifa na uhuru
wa kujieleza na kutoa maoni yake.
“Tanzania iliridhia mkataba wa umoja wa
mataifa wa haki za kiraia na kisiasa wa mwaka 1966 na juni 1976 ambapo ibara ya
19(1) inaeleza kuwa kila mtu anahaki kuwa na maoni yake bila kuingiliwa, kila
mtu ana haki ya kujieleza ikijumuisha na kuomba na kupata habari.
Prof..Kabudi amezihakikishia asasi
zisizo za kiraia na mashirika yanayosimamia Uhuru wa kujieleza na
haki ya kupata taarifa kama utekelezaji wa ibara ya 18 ya katiba.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Haki
ya Kupata Taarifa Bw. Kajubi Mukajanga amesema kuwa sheria ya ATI ilipitishwa
na kutiwa saini na Hayati Rais John Magufuli Septemba 23, 2016.
Amesema Malengo ya sheria hii ni kuwezesha
upatikanaji wa taarifa kuainisha wigo wa taarifa ambazo umma una haki ya
kuzipata kukuza uwazi na uwajibikaji wa wenye taarifa; na kuainisha mambo
mengine yahusianayo na hayo.
“Sheria hii inatoa uhai kwa haki ya kikatiba
ya kupata taarifa, na inaeleza taratibu za kutumiwa na wananchi kupata taarifa,
huku ikiweka shuruti kwa maafisa wa serikali na taasisi zinazotumia rasilimali fedha
ya umma kutoa taarifa muhimu kwa wananchi bila kusubiri kuombwa.
“Lakini pamoja na nia hii njema, uhalisia ni
kwamba utekelezaji wa sheria umekuwa ukisuasua na upatikanaji wa taarifa kwa
wananchi haujaimarishwa kama inavyokusudiwa na sheria” amesema
Tafiti zilizofanywa na taasisi za Twaweza
(2017) MCT (2019) pamoja na MISA-Tan (2020) zilibainisha kwamba raia wengi
hawana ufahamu wa sheria hii, japo wanakubali kwamba taarifa zinazoshikiliwa na
serikali ni rasilimali ya umma, amesema Mwenyekiti huyo.
Comments
Post a Comment