WAZIRI KABUDI AAHIDI KUWEKA MAZINGIRA RAFIKI KWA WANANCHI KUFIKIA VYOMBO VYA HAKI
Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi (katikati mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa wizara na viongozi wa shirika la mtandao wa watetezi wa haki za binadamu walipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi akiongea na viongozi wa shirika la mtandao wa watetezi wa haki za binadamu walipomtembelea ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.
SERIKALI
imesema itaendelea kushirikiana na wadau wa kutetea Haki za binadamu ili
kuhakikisha wananchi wanapata haki kama ilivyo ainishwa katika katiba na ilani
ya Chama cha Mapindizi (CCM) 2020/2025.
Akizungumza na viongozi
wa Mtandao wa Kutetea Mashirika yanayotetea haki za Binadamu (THRDC) Waziri wa
Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi amesema Serikali ipo tayari
kushirikiana na wadau wa kutetea haki za binadamu kwenye masuala ya kupigania
haki za msingi.
“Tuko tayari
kushirikiana na wadau ninyi muhimu kwenye masuala ya kupigania haki za wananchi
tunajua kuwa mtakua na vipaumbele vyenu muhimu na serikali pia itakuwa na
vipengele vyake ambavyo vinalenga kukuza haki za binadamu nakuleta maendeleo
katika nchi yetu.
“Hayo yote ni matakwa
ya ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 kuwa serikali imeahidi kuheshimu na
kuzingatia haki za binadamu kwa mtu mmoja mmoja, makundi na makundi ili kujenga
jamii yenye usawa,” alieleza kabudi.
Aidha alisema Tanzania
sio nchi yakufundishwa kupigania haki za binadamu kwani ni suala ambalo
lilianza tangu zamani sana na kila kitu kimeandikwa kwenye katiba.
Kwa Upande wake
Mratibu wa Mtandao wa THRDC Bw. Onesmo Olengurumwa alisema serikali inatambua
kuwa mfumo bora wa sheria ndio msingi wa kutekeleza matakwa ya katiba, Sera, na
mpango wa nchi.
Alisema asasi za
kutetea haki za binadamu zimekuwa na mchango mkubwa kwa jamii ikiwa ni pamoja
na kuhakikisha wananchi wanapata haki zao kwa wakati.
“Asasi za kiraia
zimekuwa zikifanya vizuri sana hapa nchini tunaomba serikali itambue mchango wa
asasi hizo na kuongeza ushirikiano ili ziendelee kufanya vizuri kwa maendeleo
ya wananchi na Taifa kwa ujumla,” alisema.
Olengurumwa
aliihakikishia serikali kuwa mashirika ya kutetea haki za binadamu yataendelea
kushirikiana na serikali ili kuhakikisha wananchi wanapata haki zao kwa wakati
bila vipingamizi vyovyote.
Comments
Post a Comment