WIZARA YA KATIBA NA SHERIA YATINGA 16 BORA MICHUANO YA SHIMIWI
Timu ya mpira wa miguu ya Wizara ya Katiba na Sheria imefanikiwa kuingia hatua ya kumi na sita bora
mara baada ya kuisambaratisha timu ya TARURA
asubuhi ya leo kwa jumla ya goli 4 kwa bila kwenye michuano ya SHIMIWI inayoendelea mkoani Morogoro. Aidha, timu ya kuvuta
kamba ya Wanawake nayo imeingia hatua ya kumi na sita bora huku timu ya mpira
wa pete ikisubiri hatma yake kwenye mchezo uliobaki. Ikumbukwe kuwa timu za
Sheria zilikuwa kwenye makundi yenye timu nyingi Hivyo mchujo wake unapitia
hatua za kumi na sita bora tofauti na makundi mengine ambayo yapo hatua ya robo
fainali.
Pichani juu kikosi cha timu ya mpira wa miguu cha Katiba na Sheria
kilichoisambaratisha TARURA asubuhi ya leo kwa jumla ya goli 4-0.
Pichani juu wachezaji wa Katiba na Sheria wakipata mawaidha ya kocha kipindi cha mapumziko baada ya dakika 45 za mchezo
dhidi ya TARURA.
Pichani juu makamu Mwenyekiti na Katibu wa SheriaSports Club pamoja na
Kocha wa wa timu ya mpira wa miguu wakiteta jambo kabla ya mechi.
Comments
Post a Comment