WANANCHI WANA KIU YA KUJUA SHERIA – MASHILINDI


Kaimu Meya wa Jiji la Mbeya Mhe. David Mashilindi akisaini kitabu cha wageni baada ya kutembelea banda la Wizara ya Katiba na Sheria baada ya kufunga maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria.
Kaimu Meya wa Jiji la Mbeya Mhe. David Mashilindi  ambaye ni mgeni rasmi akitoa hotuba kabla ya kufunga maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria jijini Mbeya.

Kaimu Msajili wa watoa huduma ya msaada wa kisheria Wakili Ester Msambazi akitoa taarifa ya tathmini juu ya maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria ya mwaka 2021 kwa mkoa wa Mbeya kabla ya kufungwa kwa maadhimisho hayo.

 Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Kisheria kwa Umma Wakili Griffin Mwakapeje akiongea katika hafla ya kufunga maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria jijini Mbeya.


XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX


“Maonyesho ya Wiki ya Msaada wa Kisheria yamedhihirisha kiu ya wananchi ni kubwa kutaka kujua masuala ya sheria”

Hayo yamesemwa na Kaimu Meya wa jiji la Mbeya Mhe. David Mashilindi katika hitimisho la maadhimisho ya Wiki ya Msaada wa Kisheia katika uwanja wa RuandaNzovwe jijini Mbeya ambayo yalianza Novemba 8 na yamefikia tamati Novemba 12 jijini mbeya.

Mhe Mashilindi amesema ana matumaini makubwa kuwa jamii imeelimishwa kuhusu sheria mbalimbali katika maadhimisho hayo kupitia vyombo vya habari na uwanjani ambapo elimu kuhusu mirathi, ukatili wa kijinsia , ndoa n.k imetolewa.

Aliongeza, ana imani elimu hiyo imefika kwa watendaji na wananchi kwa ujumla na hivyo kila mdau atimime wajibu wake ili wananchi wapate haki kwa ubora unaostahili.

Alisema” Juhudi mbalimbali zimefanywa kufikia wananchi lengo ni kuhakikisha  hakuna mtu anaachwa nyuma lengo likiwa ni kuboresha mfumo wa utoaji haki jinai na kila mdau atimize wajibu wake na wananchi wapate haki kwa ubora unaostahili”

Vilevile aliwataka wadau wote wa haki jinai washirikiane na wasiwe vyanzo vya migogoro mahakamani na wadaiana wanapokuwa tayari kumaliza kesi nje ya mahakama wasaidiwe.

Aidha, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba naSheria ambaye ni Mkujrugenzi wa Idara ya Huduma za Kisheria kwa Umma Bw. Griffin Mwakapeje amesema Wizara ya Katiba na Sheria inaimarisha mifumo ya kisheria na kuimarisha sera ya haki jinai.

Aliongeza  marekebisho ya sharia ya mwenendo wa mashauri ya jinai yamefanyika ikiwemo makosa ya faini kulipishwa faini ili kutimiza lengo la Rais ambalo ni kuhakikisha mashauri ya makosa ya jinai yanamalizika kwa haraka ili kupunguza msongamano magerezani.

Vilevile Kaimu Katibu Mkuu huyo alitoa rai kwa wananchi wanapopata changamoto za kisheria kwenda kwa wasaidizi wa kisheria ili kuweza kushughulikiwa matatizo yao kwa wakati na sio kukimbilia kwa watawala.

Naye Kaimu Msajili wa Wasaidizi wa Kisheria Bi. Ester Msambazi akitoa tathmini ya mafanikio yaliyopatikana katika maadhimisho hayo kwa mwaka 2021 amesema elimu na msaada wa kisheria uliotolewa maeneo ya vizuizi umewezesha mahabusu kupata dhamana na hivyo kupunguza msongamano na kuwezesha mahabusu hao kuendelea na shughuli zao za uzalishaji mali ambazo zitasaidia kukuza uchumi wa nchi.


Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA