Posts
Showing posts from May, 2022
TUNATAKA KUONA MALENGO YA MFUMO WA UANGALIZI WA UTAJIRI WA ASILI NA MALIASILIA ZA NCHI YANAFIKIWA: KATIBU MKUU WA WIZARA YA KATIBA NA SHERI
- Get link
- Other Apps
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo akifunga kikao kazi cha wataalam cha kufanya mapitio ya mfumo wa Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Maliasilia za Nchi. Picha ya pamoja. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo ,ameitaka sekretariati inayosimamia utengenezaji wa mfumo wa Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Maliasilia za Nchi inafanya kazi hiyo ipasavyo ili mfumo huo ukamilike kwa wakati na malengo yake yafikiwe, Bi. Makondo ametoa agizo hilo Mei 25, 2022 mkoani Morogoro wakati akifunga Kikao kazi cha Wataalam cha kufanya mapitio ya Mfumo huo. Mfumo huo una lengo la kusaidia utambuzi wa maliasilia za nchi na kusajili Mikataba inayoingiwa kati ya Serikali na Wawekezaji kwenye eneo la maliasilia za Nchi. Akitaja faida zitokanazo na matumizi ya mifumo, Katibu Mkuu alitaja faida hizo kuwa ni pamoja na kuleta maboresho katika kutoa huduma na kutoa huduma kwa haraka. Aidha, Bi. Makondo amesisitiza kuhusu Serikali ilivyojikita
WATAALAM WABORESHA MFUMO WA KIELEKTRONIKI WA UANGALIZI WA UTAJIRI WA ASILI NA MALIASILIA ZA NCH
- Get link
- Other Apps
WAZIRI NDUMBARO: USULUHISHI WA MIGOGORO NJE YA MAHAKAMA KUBORESHA MAZINGIRA YA UWEKEZAJI NA BIASHARA TANZANIA
- Get link
- Other Apps
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro leo akizungumza jijini Dar Es Salaam kwenye hoteli ya Lamada wakati akifungua mkutano wa siku 3 wa masuala ya haki na usuluhioshi wa migogoro ya kibiashara barani Afrika kwa njia mbadala. Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatib Kazungu akizungumza jijini Dar Es Salaam alipokuwa akimkaribisha waziri Dkt. Damas Ndumbaro kwenye hoteli ya Lamada ili kuzungumza na kufungua mkutano wa siku 3 wa masuala ya haki na usuluhioshi wa migogoro ya kibiashara barani Afrika kwa njia mbadala. Picha ya pamoja Baadhi ya washiriki wa kikao.
MAFUNZO ELEKEZI KWA BODI YA KITAIFA YA USHAURI WA MSAADA WA KISHERIA
- Get link
- Other Apps
WANAHABARI WAJENGEWA UWEZO WA NAMNA YA UTOAJI TAARIFA ZA UKATILI WA KIJINSIA.
- Get link
- Other Apps
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo akiongea na Wahariri na Waandishi wa habari wanaohudhuria mafunzo ya namna ya utoaji wa taarifa za ukatili wa kijinsia , leo 17 Mei, 2022. katika ukumbi wa Mt. Meru Arusha. Mkurugenzi wa Idara ya Utoaji Huduma za Kisheria Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Griffin Mwakapeje akitoa salamu za ukaribisho kwa mgeni Rasmi na Wahariri na Waandishi wa Habari wanaohudhuria mafunzo ya namna ya utoaji taarifa za ukatili wa kijinsia, leo 17 Mei, 2022 katika ukumbi wa Mt. Meru Arusha. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Katibu Mkuu wa Katiba na Sheria, Bi. Mary Makondo amefungua mafunzo ya siku mbili ya namna ya utoaji taarifa za ukatili wa kijinsia kwa Wahariri na Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini. Mafunzo hayo yameanza leo tarehe 17 Mei, 2022 Jijini Arusha. Akifungua mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Makondo amesema lengo la mafunzo ni kujengeana uwezo, kujifunza, kubadilishana uzoefu, mbin
MIAKA 10 YA MUUNGANO WA WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU TANZANIA (THRDC)
- Get link
- Other Apps
DKT. KAZUNGU AFUNGUA KIKAO KAZI CHA KUHAKIKI RASIMU YA MPANGO KAZI WA PILI WA KITAIFA WA HAKI ZA BINADAMU
- Get link
- Other Apps
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu amefungua Kikao Kazi cha kuhakiki Rasimu ya Mpango Kazi wa Pili wa Kitaifa wa Haki za Binadamu leo tarehe 10 Mei, 2022, Jijini Dar es Salaam. Madhumuni ya Mpango Kazi wa Kitaifa wa Haki za Binadamu ni pamoja na kuwa na mwongozo kwenye masuala ya haki za binadamu na haki za watu. “Mpango kazi huu una malengo ya kukuza, kulinda na kuheshimu haki za binadamu na watu na hatimae kuleta tija katika maendeleo ya watu na nchi.” alisema Dkt. Kazungu Mpango Kazi wa Kitaifa wa Haki za Binadamu ni mwitikio wa mapendekezo yaliyotolewa na Mkutano wa Dunia kuhusiana na Haki za Binadamu uliofanyika huko Vienna mwaka 1993 "Vienna Declaration and Program of Action" Kikao hiki kimehudhuriwa na wawakilishi wa Asasi za Kiraia na Watetezi wa Haki za Binadamu kutoka Tanzania Bara na Tanzania Visiwani kwa lengo la kupitia rasimu ya Mpango kazi wa
WAZIRI NDUMBARO AKIWASILISHA BUNGENI HOTUBA YA MAKADIRIO YA BAJETI YA MWAKA 2022/2023
- Get link
- Other Apps
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amewasilisha Bungeni Mapitio ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa mwaka 2021/22 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2022/2023. Akiwasilisha hotuba hiyo Bungeni leo Aprili 28, 2022, Dkt. Ndumbaro alisema mafanikio yaliyopatikana katika Wizara ni pamoja na kuimarisha mfumo wa utoaji nchini kwa kutumia lugha ya Kiswahili katika uandishi wa sheria na shughuli za utoaji haki mahakamani; kuongezeka kwa wigo wa mfumo wa utoaji haki kwa kuwawezesha Mawakili wa Serikali kuanza kutoa huduma za uwakili katika Mahakama za Mwanzo. Aidha, Dkt. Ndumbaro alisema Serikali imeimarisha mfumo wa utatuzi wa migogoro nje ya mahakama kwa kutumia njia mbadala ambazo ni; majadiliano, maridhiano, upatanishi na usuluhishi; kuendelea na matumizi ya lugha ya Kiswahili katika shughuli za Mahakama na uandishi wa nyaraka za kisheria ambao umeongeza uelewa w
WAZIRI NDUMBARO AFUNGUA MKUTANO WA MWAKA WA RED CROSS
- Get link
- Other Apps
KM KATIBA NA SHERIA AZINDUA BARAZA JIPYA LA WAFANYAKAZI IJA
- Get link
- Other Apps
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Bi. Mary Makondo akizindua Baraza la Wafanyakazi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto, Uzinduzi huo umefanyika Mei 5, 2022. Bi. Makondo ametoa pongezi kwa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto kwa kuwa miongoni mwa taasisi chache zinazoongoza nchini kuendesha mafunzo kwa njia ya Mtandao. Bi. Makondo ameahidi kuwa Wizara anayoiongoza iko tayari kutoa ushirikiano unaostahili kwa Chuo wakati wowote watakapouhitaji. Aidha, Ã litumia hafla hiyo kutoa wito kwa waajiri wote wanaoajiri wanasheria katika utumishi wa umma kuwapeleka watumishi hao kupata mafunzo katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto kwa mujibu wa matakwa ya Waraka wa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Waraka Namba 5 wa mwaka 2012. Hafla hiyo ya uzinduzi ilikamilika kwa wajumbe kupewa mafunzo ya siku moja ya Haki na Wajibu wa Mtumishi wa Umma pamoja na Ma
FAINI ZA MAHAKAMANI ZIWE CHANZO CHA MFUKO WA MSAADA WA KISHERIA
- Get link
- Other Apps
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt Damas Ndumbaro ametaka faini zinazolipwa mahakamani ziwe chanzo cha fedha katika mfuko wa msaada wa kisheria unaotarajiwa kuanzishwa hivi karibuni. Waziri Ndumbaro ameyasema hayo, leo tarehe 25 Aprili, 2022, jijini Dodoma wakati akipokea taarifa ya Kongamano la msaada wa Kisheria lililofanyika mapema mwezi wa nne jijini Dodoma. Taarifa imewasilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Legal Service Facility Bi. Lulu Ng’wanakilala Waziri Ndumbaro alisema “Moja kati ya chanzo cha fedha za mfuko wa msaada wa kisheria ni faini zinazolipwa mahakamani” Pia Waziri Ndumbaro aliwataka watendaji wa LSF na Wizara kujifunza kuhusu uendeshwaji wa Mfuko wa msaada wa Kisheria kutoka kwa nchi nyingine kama Kenya na Zambia ambazo tayari zina mifuko hiyo. Vilevile Waziri Ndumbaro ameshauri kuangaliwa upya kwa mfumo wa haki jinai nchini kwani unaonekana kup