DKT. KAZUNGU AFUNGUA KIKAO KAZI CHA KUHAKIKI RASIMU YA MPANGO KAZI WA PILI WA KITAIFA WA HAKI ZA BINADAMU
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Dkt.
Khatibu Kazungu amefungua Kikao Kazi cha kuhakiki Rasimu ya Mpango Kazi wa Pili
wa Kitaifa wa Haki za Binadamu leo tarehe 10 Mei, 2022, Jijini Dar es Salaam.
Madhumuni ya Mpango Kazi wa Kitaifa wa Haki za
Binadamu ni pamoja na kuwa na mwongozo kwenye masuala ya haki za binadamu na
haki za watu.
“Mpango kazi huu una malengo ya kukuza, kulinda na
kuheshimu haki za binadamu na watu na hatimae kuleta tija katika maendeleo ya
watu na nchi.” alisema Dkt. Kazungu
Mpango Kazi wa Kitaifa wa Haki za Binadamu ni
mwitikio wa mapendekezo yaliyotolewa na Mkutano wa Dunia kuhusiana na Haki za
Binadamu uliofanyika huko Vienna mwaka 1993 "Vienna Declaration and
Program of Action"
Kikao hiki kimehudhuriwa na wawakilishi wa Asasi
za Kiraia na Watetezi wa Haki za Binadamu kutoka Tanzania Bara na Tanzania
Visiwani kwa lengo la kupitia rasimu ya Mpango kazi wa pili wa Kitaifa wa Haki
za Binadamu na kutoa maoni ya kuboresha Mpango Kazi huo.
Hatua hii ya kutoa maoni ni awamu ya pili ya
kukamilisha uandaaji wa Mpango Kazi. Mpango unaandaliwa kwa kuzingatia hatua
tano; hatua zingine ni Uandaaji, Utekelezaji, Ufuatiliaji na hatua ya mwisho ni
kufanya tathmini. Wakati Wizara ya Katiba na Sheria inaratibu uandaaji na
utekelezaji wa Mpango kazi huu, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
itakuwa inafanya tathmini na ufuatiliaji.
Dkt. Kazungu ameyataja masuala yafuatayo kama
vipaumbele kwenye Mpango; Haki za Kiraia na Kisiasa; Haki za Kiuchumi,
Kiutamaduni na Kijamii (elimu, afya na maendeleo); Haki za Makundi Maalum
(Watoto, wanawake, watu wenye ulemavu na wazee)
Comments
Post a Comment