FAINI ZA MAHAKAMANI ZIWE CHANZO CHA MFUKO WA MSAADA WA KISHERIA
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt Damas Ndumbaro
ametaka faini zinazolipwa mahakamani ziwe chanzo cha fedha katika mfuko wa
msaada wa kisheria unaotarajiwa kuanzishwa hivi karibuni.
Waziri Ndumbaro ameyasema hayo, leo tarehe 25
Aprili, 2022, jijini Dodoma wakati akipokea taarifa ya Kongamano la msaada wa
Kisheria lililofanyika mapema mwezi wa nne jijini Dodoma. Taarifa imewasilishwa
na Mkurugenzi Mtendaji wa Legal Service Facility Bi. Lulu Ng’wanakilala
Waziri Ndumbaro alisema “Moja kati ya chanzo cha
fedha za mfuko wa msaada wa kisheria ni faini zinazolipwa mahakamani”
Pia Waziri Ndumbaro aliwataka watendaji wa LSF na
Wizara kujifunza kuhusu uendeshwaji wa Mfuko wa msaada wa Kisheria kutoka kwa
nchi nyingine kama Kenya na Zambia ambazo tayari zina mifuko hiyo.
Vilevile Waziri Ndumbaro ameshauri kuangaliwa upya
kwa mfumo wa haki jinai nchini kwani unaonekana kupitwa na wakati.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Legal Service Facility
Bi. Lulu Ng’wanakilala amesema wamekuwa wakishirikiana kwa karibu na Wizara ya
Katiba na Sheria tangu kuanzishwa kwa sheria ya Msaada wa Kisheria mwaka 2017
katika kuwawezesha watoaji wa msaada wa kisheria ili waweze kutenda kazi zao.
Comments
Post a Comment