KM KATIBA NA SHERIA AZINDUA BARAZA JIPYA LA WAFANYAKAZI IJA
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Katibu Mkuu Wizara ya
Katiba na Sheria, Bi. Mary Makondo akizindua Baraza la Wafanyakazi wa Chuo cha
Uongozi wa Mahakama Lushoto, Uzinduzi huo umefanyika Mei 5, 2022.
Bi. Makondo ametoa pongezi kwa Chuo cha Uongozi wa
Mahakama Lushoto kwa kuwa miongoni mwa taasisi chache zinazoongoza nchini
kuendesha mafunzo kwa njia ya Mtandao.
Bi. Makondo ameahidi kuwa Wizara anayoiongoza iko
tayari kutoa ushirikiano unaostahili kwa Chuo wakati wowote watakapouhitaji.
Aidha, àlitumia hafla hiyo kutoa wito kwa waajiri
wote wanaoajiri wanasheria katika utumishi wa umma kuwapeleka watumishi hao
kupata mafunzo katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto kwa mujibu wa
matakwa ya Waraka wa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma,
Waraka Namba 5 wa mwaka 2012.
Hafla hiyo ya uzinduzi ilikamilika kwa wajumbe
kupewa mafunzo ya siku moja ya Haki na Wajibu wa Mtumishi wa Umma pamoja na
Maadili ya Utumishi wa Umma mafunzo ambayo yameendeshwa na wawezeshaji wabobezi
kutoka Ofisi ya Raisi Menejimenti ya Utumishi ya Umma.
Lengo la mafunzo hayo ni kuleta tija kwa
watumishi, taasisi na taifa ili kuweza kukabiliana na changamoto
zitakazojitokeza katika utumishi wa mma kwa kuwa Baraza la wafanyakazi ni kioo
na mwanga wa taasisi
Comments
Post a Comment