WAZIRI NDUMBARO AKIWASILISHA BUNGENI HOTUBA YA MAKADIRIO YA BAJETI YA MWAKA 2022/2023


                                                 xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amewasilisha Bungeni Mapitio ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa mwaka 2021/22 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2022/2023.

Akiwasilisha hotuba hiyo Bungeni leo Aprili 28, 2022, Dkt. Ndumbaro alisema mafanikio yaliyopatikana katika Wizara ni pamoja na kuimarisha mfumo wa utoaji nchini kwa kutumia lugha ya Kiswahili katika uandishi wa sheria na shughuli za utoaji haki mahakamani; kuongezeka kwa wigo wa mfumo wa utoaji haki kwa kuwawezesha Mawakili wa Serikali kuanza kutoa huduma za uwakili katika Mahakama za Mwanzo.

Aidha, Dkt. Ndumbaro alisema Serikali imeimarisha mfumo wa utatuzi wa migogoro nje ya mahakama kwa kutumia njia mbadala ambazo ni; majadiliano, maridhiano, upatanishi na usuluhishi; kuendelea na matumizi ya lugha ya Kiswahili katika shughuli za Mahakama na uandishi wa nyaraka za kisheria ambao umeongeza uelewa wa sheria kwa wananchi na hivyo kurahisisha upatikanaji wa haki kwa wakati na kwa gharama nafuu.

Dkt. Ndumbaro aliongezea kuwa kuunganishwa kwa Mfumo wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini na Mahakama imerahisisha uhakiki wa amri za Mahakama kupitia njia ya mtandao.

Baada ya majadiliano Bunge limeidhinisha jumla ya Shilingi 272,768,278,800.00  kwa ajili ya matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo.

 

 

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA