BAADHI YA MAMBO KWENYE MFUMO WA HAKI JINAI YAMEPITWA NA WAKATI – WAZIRI NDUMBARO
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amesema mfumo wetu wa haki jinai ni mzuri lakini kuna baadhi ya mambo yamepitwa na wakati ukilinganisha na uhalisia, hivyo ni vema mfumo uangaliwe upya kwa kushirikiana na wadau.
Dkt.
Ndumbaro ameyasema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi wa
Kituo Cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) ofisini kwake jijini Dodoma leo
Juni 1, 2022.
Dkt.
Ndumbaro alisema “Mfumo wa haki jinai unatusaidia lakini baadhi ya mambo
yamepitwa na wakati”
Awali,
Mwenyekiti wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Bi. Anna Henga
alisema ni muhimu Serikali ikafanya maboresho ya mfumo wa Haki Jinai kwani
mfumo uliopo sasa unasababisha kesi kuchukua muda mrefu na mahabusu
kulundikana.
Bi
Henga alisema “Kuanzia Mwaka 2020 hadi 2022 mahabusu ni wengi kuliko wafungwa
kwani mahabusu wengi hawapewi dhamana na hivyo kusababisha mlundikano
magerezani”
Kituo
cha Sheria na Haki za Binadamu ni kituo kikubwa zaidi kinachotoa msaada wa
kisheria na kinahudumia watu sio chini ya 150 kwa siku, pia kina waangalizi wa
haki za Binadamu wilaya zote nchini.
Comments
Post a Comment