SERIKALI YAJIPANGA KUBORESHA MFUMO WA HAKI JINAI
Picha ya pamoja.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Serikali
imejipanga kuboresha Mfumo wa Haki Jinai nchini kwa kubaini changamoto na
kupendekeza maboresho katika mnyororo mzima wa haki jinai. Hayo yamebainishwa
katika Kikao kazi kilichoandaliwa na Wizara ya Katiba na Sheria kwa
kushirikiana na Wadau wa Haki jinai nchini. Kikao kazi hicho cha siku tano
kimefunguliwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu
Kazungu leo tarehe 13 Juni, 2022 Jijini Dodoma.
Dkt.
Kazungu amewataka Wadau wa haki jinai kujadili changamoto zinazoukabili
mnyororo mzima wa haki jinai na kupendekeza namna bora ya kuboresha mfumo huo
ili kujenga mfumo madhubuti wa sheria unaoaminika na jamii katika utoaji haki.
Maoni yatakayotolewa katika kikao kazi hiki yatatumika kuboresha Andiko la
Mapendekezo ya Maboresho ya Mfumo wa Haki Jinai Nchini kwa Mwaka wa Fedha
2022/23 hadi 2026/27.
Aidha,
Dkt. Kazungu amesema mabadiliko ya mfumo wa haki jinai yamekuja wakati muafaka
kwani hayo yamekuwa moja ya maono ya Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas
Ndumbaro tangu alipoteuliwa kuongoza Wizara hiyo.
Comments
Post a Comment