UENDESHAJI WA MASHAURI UFUATE HAKI – KATIBU MKUU MAKONDO

 Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Issa Ng’imba akifungua kikao kazi.
 

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

Kukosekana  usawa na haki katika uendeshaji wa mashauri kunaweza kusababisha wanaostahili kuipata haki kunyimwa fursa hiyo ama mtu kupewa haki asiyostahili.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Issa Ng’imba wakati akisoma hotuba kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Mary Makondo ya ufunguzi wa kikao kazi cha kuandaa hadidu rejea za kazi ya tathmini ya hali halisi ya uendeshaji wa mashauri makubwa ya rushwa. Kikao kazi hicho kimefunguliwa Juni 21, 2022, Mkoani Singida.

“Suala la usawa na haki katika uendeshaji wa mashauri ya jinai nchini ni suala la msingi linalowezesha haki kupatikana kwa kuzingatia matakwa ya Sheria nchini” Bw. Ng’imba alisema.

Aliongeza, “Wizara imeandaa kikao hiki ili wadau wa haki jinai mjadili kwa kina  dhana ya kufanya tathmini ya uendeshaji wa mashauri makubwa kama inazingatia viashiria vya uhuru na haki sawa”.

Aidha alisisitiza kuwa kupitia kikao hicho ni matarajio yake kuwa zitaandaliwa hadidu rejea zitakazotumika na Wizara kuipata Taasisi huru itakayofanya tathmini ya uendeshaji wa mashauri makubwa ya rushwa nchini.

Vilevile Bw. Ng’imba alitoa shukrani zake za dhati kwa Serikali ya Uingereza kwa kuendelea kuiunga mkono Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kusaidia juhudi za kupambana na Rushwa Nchini kupitia mradi wa kujenga uwezo wa Taasisi wa kupambana na rushwa nchini (BSAAT).

Alisema, “Natambua kuwa ufadhili unaotolewa kupitia mradi wa BSAAT umeiwezesha Wizara kuendelea kuratibu maboresho ya Mfumo wa haki Jinai yanayolenga kuimarisha upatikanaji wa Haki Jinai Nchini kwa kuzingatia Uhuru  na Haki sawa kwa pande zote zinazohusika na mashauri ya jinai nchini”. 

 

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YAIPONGEZA WIZARA KWA UTEKELEZAJI WA MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN

TUFANYE KAZI KWA UADILIFU NA USHIRIKIANO - MHE CHANA