VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA WAWAHAKIKISHIA USHIRIKIANO TLS.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro(Mb) amewahakikishia
Baraza la Uongozi la Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) ushirikiano
kutoka Serikalini kupitia Wizara ya Katiba na Sheria.
Dkt. Ndumbaro ameyasema hayo leo tarehe 24 Juni, 2022 Jijini Dodoma,
wakati wa mazungumzo na Baraza la Uongozi la Chama cha Wanasheria wa Tanganyika
wakiongozwa na Rais wa chama hicho, Prof. Edward Hosea.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Geofrey pinda amewapongeza
viongozi wa TLS kwa kuaminiwa na kuwataka wawatumikie wanachama kwa juhudi na
ubunifu ili kuleta mabadiliko chanya.
Naye Katibu Mkuu, Bi. Mary Mkondo amesema milango ya Wizara ipo wazi
muda wote kwa jambo lolote litakalo hitaji ushirikiano ili kuleta maendeleo kwa
wananchi na kuzingatia Haki.
Rais wa TLS, Prof. Edward Hosea ameishukuru Serikali kwa utayari wake wa
kushirikiana TLS katika mambo mbalimbali yaliyo ainishwa kweye kikao hicho,
ikiwa ni pamoja na kutoa huduma ya msaada wa kisheria na maendelea ya kituo cha
pamoja cha usuluhishi.
Comments
Post a Comment