KATIBU MKUU MAKONDO AFUNGUA MAFUNZO YA MFUMO WA MANUNUZI KWA MENEJIMENTI YA WIZARA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Mary Makondo akifungua Mafunzo ya Kutumia Mfumo wa Manunuzi (TANePS) kwa Bodi ya Zabuni na Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria, leo tarehe 11 Julai, 2022 Jijini Dar es Salaam.
Mafunzo hayo ambayo yatafanyika hadi tarehe 15 Julai, 2022 ni ya kuwajengea Uwezo Wakuu wa Idara na Vitengo katika masuala ya matumizi ya Mfumo wa Manunuzi. Katibu Mkuu Makondo alitoa maelekezo kwa Washiriki kuhakikisha wanayatumia Mafunzo hayo kujifunza na kushiriki kikamilifu kwa kutumia uzoefu wao katika kazi na matumizi ya mfumo katika kusaidia shughuli za Serikali.
Comments
Post a Comment